Ndugu na dada zangu. Mbio za Maisha



Similar documents
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA BILL SUPPLEMENT

TUNGO ZA KUJIBIZANA: "KUAMBIZANA NI SIFA YA KUPENDANA"t

MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

Linking Adult Education with Formal Schooling in Tanzania: Mission Unfulfilled

Annual Report and Financial Statements

Contents Page. 3. Financial Highlights 4-8. Chairman s Statement CEO s Statement

THE OIL AND GAS REVENUES MANAGEMENT ACT, 2015 ARRANGEMENT OF SECTIONS PART I PRELIMINARY PROVISIONS PART II ADMINISTRATIVE PROVISIONS

Ni Wakati Wa Kuamka! Ellis P. Forsman. Ni Wakati Wa Kuamka (It's Time To Wake Up) 1

EXISTENTIALISM AND FEMINISM IN KEZILAHABI S NOVEL KICHWAMAJI

TANZANIA COFFEE BOARD VACANCIES ANNOUNCEMENT

MARX'S SHORTS AND ANCESTORS' CAVES: TRACING CRITICAL MOTIFS IN KEZILAHABI'S PLAY AND POEMS*

Contents. CORE VALUES Integrity Professionalism Team Spirit Safety Culture. Company Information 2 Message from the Chairman 4

ROMAN CATHOLIC FAITH REPRESENTED IN KEZILAHABI'S MZINGILE SONJA MEZGER AAP 72 (2002) SWAHILI FORUM IX 75-85

KANISA LINAHITAJI KUJUA

Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

Toleo No. 51 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Tarehe Januari, 2015

Centum Investment Company Limited Annual Report & Financial Statements fy 13/14

Annual Report Report and and Financial Statements

Lesson 56: Business: [biashara: ununuzi, upigaji bei na uuzaji] Business: Shopping, Buying and Selling. A). Business Vocabulary.

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SABOTI CONSTITUENCY, HELD AT KITALE TOWN MUSEUM HALL

Creation of a Speech to Text System for Kiswahili

TANZANIA AND HIV/AIDS TANZANIA NA UKIMWI

OPERATIONS MANUAL FOR IMPLEMENTATION AND MANAGEMENT OF A COMMUNITY HEALTH FUND in Tanga Region

Kitabu hiki kimefanikishwa kwa msaada wa Taasisi ya Bill na Melinda Gates

DAR ES SALAAM UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION. A Constituent College of the University of Dar Es Salaam STAFF FUNERAL POLICY

KUKITANDAWAZISHA KISWAHILI KUPITIA SIMU ZA KIGANJANI: TAFAKARI KUHUSU ISIMUJAMII

Lesson 14a: Numbers and Counting

815 SWA. Health undertaking Kuwajibika Kiafya. Tafadhali weka kurasa hii ya maelezo kama kumbukumbu yako

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,

Tunza Jamii Yako, Tunza Mazingira Yako kwa Maisha Bora. Jihusishe. Jipangie. Amua

Yaliyomo. II. Dodoso la Kilimo... 62

THE ANTI-MONEY LAUNDERING ACT,2006

A SHABA SWAHILI LIFE HISTORY: TEXT AND TRANSLATION

CONTENTS. Financial Section. Sehemu ya Kiswahili. Statutory Information

Lesson 24: Adjectives

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF

Uundaji wa Istilahi za Kiswahili Kileksikografia na Athari zake S.S. SEWANGI University of Dar-es-Salaam, Tanzania

CUF. Rais makini, Serikali makini Uchumi Imara, Mabadiliko Sahihi

LEARNING HOW TO TEACH

ANNUAL REPORT 2015 THE TASKS OF TBL INTRODUCING

Tuko Pamoja. Adolescent Reproductive Health and Life Skills Curriculum

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA JAMII MKOA WA DODOMA

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK

Mwalimu Nyerere Engages His People: Scripture Translation in Swahili Verse

TEGENI MASIKIO: COMPOSING EAST AFRICAN REALITIES THROUGH YOUNG EYES

MORE SWAHILI PROVERBS FROM EAST AFRICA METHALI ZAIDI ZA KISWAHILI TOKA AFRIKA MASHARIKI. L. Kalugila. A. Y. Lodhi

KISWAHILI Pam Inoti - pamby22@gmail.com

Teach Yourself Swahili

TAARIFA YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UKIMWI MKOA WA KIGOMA

TRAINING ON ENTREPRENEURSHIP AND BUSINESS MANAGEMENT SKILLS FOR SELECTED VILLAGERS IN RUFIJI

LUGHA YA MITAANI IN TANZANIA THE POETICS AND SOCIOLOGY OF A YOUNG URBAN STYLE OF SPEAKING

Sda Church Nyimbo Za Kristo

CURRICULUM INNOVATION IN TEACHER EDUCATION

Celebration of the French «Bastille Day» Remarks by Ambassador Elisabeth Barbier 14th July 2010

Language Choice in Swahili Newspaper Advertising in Tanzania

1. TASAF operations steadily approaching set targets

P.O. Box 4374 DAR ES SALAAM TEL: /6 FAX:

The mother, her confidants and the prevention of mother-to-child transmission of HIV (PMTCT) services in the Kilimanjaro region, Tanzania

TEKNOLOJIA ZA UTAYARISHAJI, USINDIKAJI NA HIFADHI YA MAZAO YA MBEGU ZA MAFUTA BAADA YA KUVUNA. Kitabu Namba 5

DR. HAMISI O. BABUSA (PHD)

Promoting Regional Trade to Enhance Food Security

Mother Tongue Theological Education in Africa: A Response to Jim Harries The Prospects for Mother Tongue Theological Education in Western Kenya

MEANING AS USE: A FUNCTIONAL VIEW OF SEMANTICS AND PRAGMATICS

Ambassador s Community Grants Fund for HIV/AIDS Relief

Swahili. Information provided by: National African Language Resource Center (NALRC)

The Mosaic Project Theme Song 2001 The Mosaic Project Music by Brett Dennen, Lyrics by Brett Dennen and Lara Mendel

ARMS CONTROL Volume 3 Issue 1 May 2011

Lesson 43: Commands. D). Commands may take object markers to indicate the recipient of a command

The Usage of Kiswahili in Blog Discourse and the Effect on Its Development

Section 2 Assessment

Integrated Logistics System (ILS) Procedures Manual

The United Republic of Tanzania

Winners, cheats and witches: East African soccer cartoons Beez, Jigal

NEGOTIATING THE NEW TUKI ENGLISH-SW AHILI DICTIONARY A CRITIQUE FROM A PEDAGOGICAL AND SCHOLARLY PERSPECTIVE'

Towards Full Comprehension of Swahili Natural Language Statements for Database Querying

INITIAL BEHAVIOR CHANGE COMMUNICATION (BCC) INTERVENTIONS EFFECTIVENESS EVALUATION REPORT

CURRICULUM VITAE PERSONAL DETAILS. Prof. Wanyama Mellitus Nyongesa. Age: 47. Associate Professor of Musicology at Moi University, Eldoret, Kenya

TANZANIA PARALEGAL BASELINE SURVEY


Tense and aspect in Swahili

The Nguzo Saba of the seven days of Kwanzaa:

LIN892: Distributed Morphology

L E A P n e w s. Tahariri. Editor s note. Number 15/16 September December 2007 Newsletter of the Language in Education in Africa Project

Chapter 4 Service Design

ACADRI 2015 TRAINING PROGRAMMES

Girls Getting to Secondary School Safely: Combating Gender-based Violence in the Transportation Sector in Tanzania

Lesson 9: Swahili Noun Classes

V-TO-I MOVEMENT IN KISWAHILI

Vidunda (G38) as an Endangered Language?

ก ก ก ก Hydrologic Cycle

The Story of Swahili

MOSHI UNIVERSITY COLLEGE OF CO-OPERATIVE AND BUSINESS STUDIES (MUCCoBS) A Constituent College of Sokoine University of Agriculture


Primary Care Plus Enrollment Booklet

Headline News Analysis. Top-Ranking Headline Stories

KAMUSI YA KISWAHILI SANIFU IN TEST: A COMPUTER SYSTEM FOR ANALYZING DICTIONARIES AND FOR RETRIEVING LEXICAL DATA

What Children & Young People are Saying about Poverty in Tanzania 0

GLOBAL HEALTH SUMMER PROGRAM HANDBOOK MOSHI, TANZANIA CORNELL UNIVERSITY GLOBAL HEALTH PROGRAM. Photograph taken by Rebecca Stoltzfus


CURRICULUM VITAE. 1. SUMMARY OF EXPERIENCE Special Needs Education Lecturer Psycho-educational Assessment Professional

Transcription:

UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2012 Na Rais Thomas S. Monson Mbio za Maisha Sisi tulitoka wapi? Kwa nini tuko hapa? Tutaenda wapi baada ya maisha haya? Haya maswali ya kawaida hayafai kubaki bila kujibiwa. Ndugu na dada zangu wapendwa, asubuhi hii ningependa kuwambia ninyi kweli za milele hizo kweli ambazo zinaimarisha maisha yetu na kutupeleka nyumbani salama. Kila mahali, watu wako mbioni. Ndege za jeti zinaharikisha mizigo yake ya binadamu ya thamani kuvuka bara pana na bahari kuu ili kwamba mikutano ya biashara iweze kufanyika, majukumu yatendeke, likizo zifanyike, na familia kutembelewa. Barabara kila mahali ikijumuisha baraste, baraste kuu hupitia mamilioni ya magari, yanayobeba mamilioni zaidi ya watu, katika mfulululizo unaonekana kutokwisha na kwa sababu nyingi sana tunapuruka katika shughuli kila siku. Katika mwendo huu wa harakaharaka wa maisha je! Tunatua na kwa muda kutaamali hata mawazo ya kweli za milele? Tunapolinganisha kweli za milele, maswali mengi ya maisha na mambo ya kila siku kwa kweli ni ya maana kidogo sana. Ni nini tutakula njioni? Ni rangi gani tutapaka sebuleni? Je! Tumsajili Johnny kwa kandanda? Maswali haya na mengine mengi kama haya hufifia katika umuhimu wake wakati matatizo yanapoibuka, wakati wapendwa wetu wanapoumia au kujeruhiwa, wakati ugonjwa unapoingia katika nyumba yenye afya, wakati mshumaa wa maisha unapofifia na giza linapotishia. Mawazo yetu yanachongwa, na kwa urahisi tunaweza kutambua kile kilicho cha muhimu hasa na kilicho duni tu. Majuzi nilimtembelea mwanamke ambaye alikuwa anapigana na ugonjwa unaotishia uzima kwa miaka miwili. Alisema kwamba kabla ya ugonjwa wake, siku zake zilijawa na shughuli kama vile kusafisha nyumba mpaka ikwatuke na kuijaza na fanicha na vyombo vya urembo. Alikwenda kwa mtengeneza nywele wake mara mbili kila wiki na kutumia fedha na muda kila wiki kuongeza mavazi yake. Wajukuu walikuwa wanaalikwa kwa uadimifu sana, kwani alikuwa na hofu kwamba kile alichofikiria kuwa mali yake ya thamani ingeweza kuvunjwa au kuharibiwa na mikono midogo isiyo na uangalifu. Na halafu akapokea habari za kustusha kwamba maisha yake yakuwa hatarini na kwamba angekuwa na maisha mafupi sana yaliyobakia. Yeye alisema kwamba wakati aliposikia utambuzi wa daktari, na alijua mara moja kwamba atatumia muda wowote uliobakia na familia yake na marafiki zake na akiwa na injili kama kitovu cha maisha yake, kwani haya yaliwakilisha kile kilichokuwa cha thamani kwake. Nyakati kama hizi banaya zinakuja kwetu sote katika wakati mmoja au mwingine, ingawa labda sio kila mara kupitia hali za kusisimua. Tunaona wazi kile ambacho kina maana katika maisha yetu na jinsi tunafaa kuishi. Mwokozi alisema: Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba; Bali jiwekeeni hazina mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala hawaibi; Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako. 1 Katika nyakati zetu za tafakari ya kina au mahitaji makuu, nafsi ya mtu uelekea mbinguni,kutafuta majibu matakatifu kwa maswali yao makuu: Je! Tulitoka wapi? Kwa nini tuko hapa? Tutaenda wapi baada ya kuacha maisha haya? Majibu ya maswali haya hayawezi kupatikana ndani ya vitabu vya usomi, kwa kutafuta katika Intaneti. Haya maswali yanashinda maisha ya muda. Yanakumbatia umilele. Je! Tulitoka wapi? Hii swali haliepukiki kufikiriwa, kama alisemwi, na kila mwanadamu. Mtume Paulo aliwaambia Wathene katika Kilima Mars kwamba sisi tu 1

wazao wa Mungu. 2 Kwa vile tunajua kwamba miili yetu ni uzao wa wazazi wetu wa kimwili, lazima tuchuguze maana ya maneno ya Paulo. Bwana alitangaza kwamba Na roho na mwili ndiyo nafsi ya mwanadamu. 3 Na hivyo ndivyo ilivyo roho uzao wa Mungu. Mwandishi wa Waebrania umuita Yeye Baba wa roho. 4 Roho za wanadamu wote kihalisi wana na mabinti Wake. 5 Tunatambua kwamba watunzi wa mashahiri wameandika, kujifunza juu ya hili jambo, wakiandika jumbe za kuvutia na kuandika mawazo ya ajabu. William Wordsworth aliandika kweli hii: Kuzaliwa kwetu ni kama kulala na kusahau; Nafsi huamuka nasi, Nyota ya maisha yetu, Ilikuwa sehemu ingine pa kuhisi Na inatoka mbali, Sio katika usahaulivu, Na sio kwa uchi kabisa, Bali twaja tufuatia mawingu ya utukufu Kutoka kwa Mungu, ambaye ndiye nyumba yetu Mbinguni ipo karibu nasi uchangani! 6 Wazazi utafakari majukumu yao ya kufunza, kuwavutia, na kuwapatia mwongozo, maelekezo na mfano. Na wazazi wakitafakari, watoto na hasa vijana wanauliza ili swali la muhimu. kwa nini tuko hapa? Kwa kawaida, linasemwa kimya nafsini na kwa njia ingine, kwa nini mimi niko hapa? Tunafaa kuwa na shukrani jinsi gani kwamba Muumba mwenye hekima aliumba ulimwengu na kutuweka hapa tukiwa na pazia ya kusahau kuwepo kwetu kwa mapema ili tuweza kupata uzoefu wa wakati wa kujaribiwa, nafasi ya kujithibitisha wenyewe, kwamba ili tuhitimu kwa yote ambayo Mungu ametutayarishia sisi kupokea. Ni wazi, madhumuni muhimu ya kuwepo kwetu juu ya ulimwengu ni kupokea mwili wa nyama na mifupa. Sisi pia tumepatiwa kipawa cha wakala. Kwa njia elfu, tuna nafasi za kuchagua wenyewe. Hapa tunajifunza kutoka kwa mchapakazi hodari wa uzoefu. Tunatambua kati ya wema na uovu. Tunatofutisha chungu na tamu. Tunagundua kuna matunda yanayoambatana na matendo yetu. Kwa kutii amri za Mungu, tunaweza kuhitimu kwa ile nyumba iliyosemwa na Yesu wakati Yeye alitamka: Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi;... maana naenda kuwaandalia mahali... ili nilipo mimi, nanyi mwepo. 7 Ingawa tunakuja katika maisha ya muda katika maisha ya duniani mawimbi yafuatayo ya utukufu, maisha yanasonga mbele bila kusita. Ujana ufuata utoto, na ukomavu huja bila kutambulika. Kutokana na uzoefu tunaojifunza haja ya kufikia mbinguni kwa usaidizi tunapotafuta njia katika mapito ya maisha. Mungu, Baba yetu, na Yesu Kristo, wameweka njia alama hadi ukamilisho. Wanatuita sisi tufuatie kweli za milele na kuwa wakamilifu, kama Wao walivyo kamili. 8 Mtume Paulo alilinganisha maisha na mbio. Kwa Waebrania aliwasihi, Tuweke kando...dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu. 9 Katika ari, tusikutilia maana ushauri wa busara kutoka kwa Mhubiri: Si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani. 10 Ninapotazama mbio za maisha, nakumbuka mbio za aina ingine, hata kutoka siku za utotoni. Marafiki zangu nami tulitwaa visu vidogo wa kukunja na, kutoka kwa mbao laini za mti maji, tulijenga mfano wa mashua ndogo. Kwa anga ya umbo la pembetatu mraba ya kitambaa cha pamba, kila mmoja wetu alishua chombo katika mashindano katika maji maasi ya Mto Provo wa Utah. Tungekimbia kwenye ukingo wa mto na kutazama vyombo vidogo wakati mwingine vikiyumbayumba sana katika mkondo wa kasi na wakati mwingine hivi vilisafiri shwari jinsi maji yalipata kina. Wakati wa mashindano fulani, tuliona kwamba mashua moja iliongoza zile zingine kuelekea mstari wa kumalizia uliyowekwa. Ghafula, mkondo unaichukua karibu sana na kizingia cha maji kikubwa, na hiyo mashua ikipinduka na kuzama. Ilizungushwazungushwa na kubebwa, isiweze kurudi katika mkondoni. Na mwishowe kutua vibaya huko katika takataka iliyoizunguka kuishikilia kwa minyiri yenye kubana ya kuvumwani ya kijani. Mfano ya mashua ya utotoni haikuwa na mkuku wa uthabiti, haikuwa na usukani wa kupatiana mwekeleo, na haikuwa na mtambo wa nguvu. Bila shaka cha safari yake kilikuwa kufuata mkondo mapito yaliyo na pingamizi kidogo. Tofauti na mifano ya mashua, sisi tumepatiwa sifa za kiasili za kutongoza katika safari yetu. Tunaingia katika maisha ya muda sio kuelea katika mikondo ivumayo ya maisha bali kwa uwezo wa kufikiria, akili, na kupata. Baba yetu wa Mbinguni Hakutushua sisi katika safari yetu ya milele bila kutupatia njia ambazo kwazo tungeweza kupokea kutoka Kwake mwongozo ili kuhakikisha kurudi kwetu salama. Naongea kuhusu maombi. Naongea pia kuhusu ushawishi kutoka kwa ile sauti ndogo, tulivu; Sijasahau maandiko matakatifu, ambayo yana neno la Bwana na maneno ya manabii yanayotupatia sisi usaidizi wa kufanikiwa kuvuka mstari wa kumaliza. Wakati fulani katika maisha yetu ya muda, kunatokeza hatua za kisitasita, tabasamu chovu, maumivu ya ugonjwa hata kuparara kwa ujana, kufikia nyakati za kupukutika, kugandamana, na uzoefu tunaouita kifo. Kila mtu wenye makini ameshajiuliza swali lililosemwa vyema na Ayubu wa kale: Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? 11 Tunaweza kujaribu kuliweka kando hilo swali, daima litarudi. Kifo huja kwa kila 2

mwanadamu. Huja kwa wazee wanapositasita miguu. Mwito wake usikika na wale ambao hawajafika haya katikati ya safari ya maisha. Nyakati zingine hunyamazisha kucheko cha watoto wadogo. Na je! Kuwepo baada ya kifo? Kifo ni mwisho wa yote? Robert Blatchford katika kitabu chake God and My Neighbor, alishambulia vikali sana imani zinazokubalika za Kikristo kama vile Mungu, Kristo, maombi na hasa maisha ya milele. Alisisitiza kwamba kifo kilikuwa mwisho wa kuishi kwetu na kwamba hakuna yeyote anayeweza kuthibitisha vingine. Kisha kitu cha kushangaza kikafanyika. Ukuta wa shaka ghafula ukabomoka hata mavumbini. Yeye akawachwa wazi na bila kinga. Pole pole akaanza kuhisi njia yake hata kwenye imani ambayo alikuwa anakejeli na kuiacha. Ni nini lichokuwa kimelete haya mabadiliko yake? Mke wake alikuwa amefariki. Kwa moyo uliovunjika alienda hadi kwenye chumba ambako mwili wa mke ulikuwa umelazwa. Akatazama tena uso wa ambao alikuwa anaupenda sana. Akitoka nje, alisema kwa rafikiye: Ni yeye na hali si yeye. Kila kitu kimebadilika. Kitu kilichokuwepo awali kumetwaliwa. Siye yule yule. Ni kitu gani kilichokwenda kama si nafsi? Baadaye aliandika: Kifo sio vile watu fulani wanavyofikiria. Ni kama vile tu kwenda katika chumba kingine. Katika hicho chumba kingine tutapata... wanawake na wanaume wapendwa na watoto wazuri tuliopenda na kupoteza. 12 Ndugu na kina dada, sisi tunajua kwamba kifo siyo kikomo. Ukweli huu umefunzwa na manabii walio hai katika nyakati zote. Pia unapatikana katika maandiko matakatifu yetu. Katika Kitabu cha Mormoni tunasoma maneno mahususi na ya kufariji: Sasa, kuhusu hali ya roho kati ya kifo na ufufuo Tazama, nimejulishwa na malaika, kwamba roho za watu wote, mara zinapotoka kwa mwili huu wa muda, ndio, roho za watu wote, zikiwa njema au ovu, zinachukuliwa nyumbani kwa yule Mungu ambaye alizipatia uhai. Na ndipo itakuja kuwa kwamba roho za wale walio haki zinapokelewa kwa hali ambayo ni ya furaha, ambayo inaitwa peponi, hali ya kupumzika, hali ya amani, ambapo zitapumzikia kutoka kwa taabu zao zote na kutoka kwa mashaka yote, na masikitiko. 13 Baada ya Mwokozi kusulubiwa na mwili Wake kulazwa katika kaburi kwa siku tatu, roho iliingia ndani tena. Jiwe lilisukumwa mbali,na Mkombozi mfufuka akaenenda mbele, amevikwa kwa mwili wa nyama na mifupa usiokufa. Jibu la swali la Ayubu, Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Lilikuja kwa Mariamu na wengine waliokwenda kwenye kaburi na kuwaona watu wawili waliokuwa na mavazi ya kumeremeta ambao wasema na wao: Kwa nini mnamtafuta aliye hai katika wafu? Hayupo hapa, amefufuka. 14 Kama matokeo ya ushindi wa Kristo dhidi ya kaburi, sisi sote tutafufuka. Huu ndio ukombozi wa nafsi. Paulo aliandika: Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali. 15 Ni utukufu wa selestia ambao tunataka. Ni katika uwepo wa Mungu tunatamani kuishi. Ni familia za milele ambazo tunataka ushiriki wake. Baraka kama hizo zinapatikana kupitia kujitahidi maishani, kutafuta, kutubu, na mwishowe kufaulu. Je! Tulitoka wapi? Je! Kwa nini tuko hapa? Je! Tutaenda wapi baada ya maisha haya? Haifai kamwe kuwa maswali haya muhimu kukosa kujibiwa. Kutoka kwa kina cha nafsi yangu na katika unyenyekevu wote, mimi nashuhudia kwamba hivi vitu vyote ambavyo nimeongea ni vya kweli. Baba yetu wa Mbinguni hufurahia kwa ajili ya wanaoweka amri Zake. Yeye anajali pia mtoto aliyepotea, kijana ajizi, kijana mpotevu, mzazi mkosaji. Kwa upole Bwana anasema na hawa, na hasa kwa wote: Njoni tena, Njoni hapa. Njoni ndani. Njoni nyumbani. Njoni kwangu. Katika wiki moja sisi tutasherekea Pasaka. Mawazo yetu yatageukia maisha ya Mwokozi, kifo Chake, ufufuko Wake. Kama shahidi maalumu Wake, nashuhudia kwenu kwamba Yeye yu hai na kwamba Yeye anangojea kurudi kwetu kwa ushindi. Kwamba kurudi kama huku kutakuwa kwetu, naomba kwa unyenyekevu hata Yesu Kristo, Mwokozi wetu na Mkombozi wetu, amina. MUHTASARI 1. Mathayo 6:19 21. 2. Matendo ya Mitume 17:29. 3. Mafundisho na Maagano 88:15. 4. Waebrania 12:9. 5. Mafundisho na Maagano 76:24. 6. William Wordsworth, Ode: Intimations of Immortality from Recollections of Early Childhood (1884), 23 24. 7. Yohana 14:2 3. 8. Ona Mathayo 5:48; 3 Nefi 12:48. 9. Waebrania 12:1. 10. Mhubiri 9:11. 11. Ayubu 14:14. 12. Ona Robert Blatchford, More Things in Heaven and Earth: Adventures in Quest of a Soul (1925), 11. 13. Alma 40:11 12. 14. Luka 24:5 6. 15. 1 Wakorintho 15:40. 3

Mafundisho ya Wakati Wetu Mafundisho ya Jumapili ya nne kwa Ukuhani wa Melkizedeki na Muungano wa Usaidizi wa Kina Mama yatatengwa kwa Mafundisho ya Wakati Wetu Kila somo linaweza kutayarishwa kutoka kwa hotuba moja au zaidi za mkutano mkuu wa hivi majuzi (ona chati hapa). Marais wa vigingi na wilaya wanaweza kuchagua hotuba zitakazotumiwa, au wanaweza kuwapa majukumu maaskofu na marais wa matawi. Viongozi wanafaa kusisitiza umuhimu wa ndugu za Ukuhani wa Melkizediki na akina dada wa Muungano wa Usaidizi wa Kina Mama kusoma hotuba sawa katika Jumapili hizo. Wale wanaohudhuria mafundisho ya Jumapili ya nne wanahimizwa kusoma na kuleta madarasani toleo la gazeti la mkutano mkuu la hivi karibuni. Mapendekezo ya Kutayarisha Somo kutoka kwa Hotuba Omba kwamba Roho Mtakatifu awe nawe unaposoma na kufundisha hotuba hizi. Unaweza kushawishika kutayarisha masomo kwa kutumia vifaa vingine, lakini hotuba za mkutano mkuu ni mtaala ulioidhinishwa. Jukumu lako ni kuwasaidia wengine kujifunza na kuishi kulingana na injili kama ilivyofundhishwa katika mkutano mkuu wa Kanisa wa hivi majuzi. Rejelea upya hotuba hizi, ukitafuta kanuni na mafundisho yanayolingana na mahitaji ya washiriki wa darasa. Pia, tafuta hadithi, marejeleo ya maandiko, na matamko kutoka kwa hotuba ambazo zitakazokusaidia kufundisha kweli hizi. Tayarisha umbo la jinsi ya kufundisha kanuni na mafundisho. Fikiria kujumuisha maswali ambayo yatawasaidia washiriki wa darasa: Angalia kanuni na mafundisho katika hotuba. Tafakari juu ya maana yake. Shiriki mawazo, tajiriba, uzoefu na shuhuda. Tumia kanuni na mafundisho haya katika maisha yao. MIEZI MASOMO YATAPOFUNZWA Aprili 2012 Oktoba 2012 Oktoba 2012 Aprili 2013 VIFAA VYA MAFUNDISHO YA JUMAPILI YA NNE Hotuba zilizotolewa katika mkutano mkuu wa Aprili 2012 * Hotuba zilizotolewa katika mkutano mkuu wa Oktoba 2012 * * Kwa Masomo ya Jumapili ya Nne ya Aprili na Oktoba, hotuba zinaweza kuchaguliwa kutoka kwa mkutano mkuu wa awali au kutoka kwa mikutano ya majuzi sana. Hotuba hizi zinapatikana (katika lugha nyingi) katika conference.lds.org. 2012 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Imechapishwa USA. Kiingereza kiliidhinishwa: 6/11. Tafsiri iliidhinishwa: 6/11. Tafsiri ya First Presidency Message, May 2012. Swahili. 10365 743 4

UJUMBE WA MWALIMU MTEMBELEZI, MEI 2012 Na Rais Henry B. Eyring Nilimsikia Rais Spencer W. Kimball katika kikao cha mkutano mkuu akiuliza kwamba Mungu ampatie milima ya kukwea. Alisema: Kuna changamoto kubwa mbele yetu, nafasi kuu za kutimizwa. Nakaribisha hayo matazamio ya kusisimua na kuhisi kusema kwa Bwana kwa unyenyekevu, Nipe mlima huu, nipe changamoto hizi. 1 Moyo wangu ulichochewa, kujua, kama nilivyojua, baadhi ya changamoto na dhiki alizokuwa amepata hapo mapema. Nilihisi hamu ya kuwa kama yeye, mtumishi shupavu wa Mungu. Basi usiku mmoja niliomba jaribio la kutathimini ujasiri wangu. Nakumbuka wazi kabisa. Jioni nilipiga magoti katika chumba changu cha kulala kwa imani ambayo ilionekana karibu kujaza moyo wangu hata upasuke. Karibu siku au siku mbili maombi yangu yalijibiwa. Jaribio gumu sana maishani mwangu lilinishangaza na kuninyenyekeza. Lilinipatia somo la pembe mbili. Kwanza, nilikuwa na thibitisho kwamba Mungu alisikia na kujibu ombi langu. Na pili, nilianza somo ambalo bado linaendelea ili kujifunza kwa nini nilihisi kujiamini kama huko usiku ule baraka kuu Mshauri wa Kwanza katika Urais wa Kwanza Milima ya Kukwea Kama tuna imani katika Yesu Kristo, nyakati ngumu vile vile nyakati rahisi katika maisha zinaweza kuwa baraka. ambayo ingetokana na dhiki ili kuwa zaidi ya fidia ya gharama yoyote. Dhiki iliyonigonga katika siku hiyo ya zamani sasa inaonekana kuwa ndogo kulingana na kile kimenijia tangu wakati huo, kwangu na kwa wale ninaowapenda. Wengi wenu sasa mnapitia majaribu ya kimwili, kiakili, na kimhemko ambayo yanawafanya kulia kama alivyofanya mtumishi mkuu na mwaminifu wa Mungu niliyemjua vyema. Muuguzi wake alimsikia akisema kwa sauti kutoka kwa kitanda chake cha maumivu: Nimejaribu katika maisha yangu yote kuwa mwema, kwa nini haya yatendeke kwangu? Mnajua jinsi Bwana alivyojibu swali hili kwa Nabii Joseph Smith katika chumba cha gereza: Na kama utatupwa ndani ya shimo, au katika mikono ya wauaji, na hukumu ya kifo ikapitishwa juu yako; kama utatupwa kilindini; kama mawimbi makali yatakula njama dhidi yako; kama upepo mkali utakuja kuwa adui yako; kama mbingu zitakusanya giza, na vitu vyote vya asili vikiungana ili kuzingira njia yako; na juu ya yote, kama mataya yale ya jahanamu yataachama kinywa wazi kwa ajili yako, fahamu wewe, mwanangu, kwamba mambo haya yote yatakupa wewe uzoefu, na yatakuwa kwa faida yako. Mwana wa Mtu amejishusha chini yao wote. Je, wewe u mkuu kuliko yeye? Kwa hiyo, shikilia njia yako, na ukuhani utabakia nawe; kwa kuwa mipaka yao imewekwa, hawawezi kuivuka. Siku zako zinafahamika, na miaka yako haitahesabika kuwa michache; kwa hiyo, usiogope mwanadamu awezacho kukutenda, kwani Mungu atakuwa pamoja nawe milele na milele. 2 Hakukuonekana kwangu jibu bora kwa swali la kwa nini majaribu huja na nini tutafanya zaidi ya maneno ya Bwana Mwenyewe, ambaye alipitia majaribu makali kwa sababu yetu kushinda vile tunaweze kufikiria. Kumbuka maneno Yake aliposhauri kwamba tunafaa, kutokana na imani katika Yeye, tutubu: Kwa sababu hii ninakuamuru wewe kutubu tubu, nisije nikakupiga kwa fimbo ya kinywa changu, na ghadhabu yangu, na kwa hasira yangu, na mateso yako kuwa machungu machungu namna gani hujui, makali namna gani hujui, ndiyo, namna gani magumu kuyavumilia hujui. Kwani tazama, Mimi, Mungu nimeteseka mambo haya kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wasiteseke kama watatubu; Lakini kama hawatatubu lazima wateseke hata kama Mimi; Mateso ambayo yalisababisha Mimi mwenyewe, hata Mungu, mkuu kuliko yote, kutetemeka kwa sababu ya maumivu, na kutoka damu kwenye kila kinyweleo, na kuteseka mwili na roho na kutamani nisinywe kikombe kichungu, na kusita Hata hivyo, utukufu na uwe 1

kwa Baba, na Mimi nikachukua na kukamilisha maandalizi yangu kwa wanadamu. 3 Wewe na mimi tuna imani kwamba njia ya kuinuka kupitia na kushinda majaribu ni kuamini kwamba kuna mafuta katika Giliadi 4 na kwamba Bwana ameahidi, sitakupungukia... sitakuacha. 5 Hivi ndio Rais Thomas S. Monson ametufunza sisi na wale tunaohudumu katika kile kinachoonekana kuwa upweke na majaribu makali. 6 Lakini Rais Monson amefunza pia kwa hekima kwamba msingi wa imani kihalisi ya zile ahadi huchukua muda kujengeka. Unaweza kuwa umeona haja ya huu msingi kama vile nimepata kuona kandoni mwa mtu aliye tayari kushindwa na vita ili kuvumilia hadi mwisho. Kama msingi wa imani haujapandwa katika mioyo yetu, uwezo wa kuvumilia utabomoka. Madhumuni yangu leo ni kuelezea kile ninachojua kuhusu jinsi tunavyoweza kuweka ule msingi usiotikisika. Nafanya hivyo kwa unyenyekevu mkuu kwa sababu mbili. Kwanza, kile nitakachosema kinaweza kuwavunja moyo wengine wenu ambao mnapambana ndani ya dhiki kubwa na kuhisi misingi yao ya imani inabomoka. Na pili, najua kwamba yale majaribu makubwa sana yapo mbele yangu kabla mwisho wa maisha. Kwa hivyo dawa ninayowapa bado haijathibitishwa katika maisha yangu mwenyewe kupitia kuvumilivu hadi mwisho. Kama kijana nilifanya kazi na kontrakta wa ujenzi wa vitako vya nyumba na msingi kwa nyumba mpya. Katika joto la majira ya joto ilikuwa vigumu kufanya kazi ya kutayarisha uwanda umbo ambalo tungemwagia simiti kwa kitako cha nyumba. Hapakuwa na mashini. Tulitumia sururu na mwiko. Kujenga msingi thabiti kwa majengo ilikuwa ni vigumu siku hizo. Pia ilihitaji subira. Baada ya kumwaga kitako cha nyumba tulingojea kikauke. Hata kwamba tulitaka kuendeleza kazi mbele, tulingojea pia kumwagia msingi kabla ya kuondoa umbo. Na kilichokuwa cha kustajabisha kwa mjenzi mgeni kilikuwa ni kile kilichoonekana kuwa kigumu na mfanyiko uliochukua muda mrefu wa kuweka vyuma ndani ya umbo ili kupatia msingi uliomalizika nguvu. Kwa njia hio hio, uwanda lazima utayarishe vyema kwa msingi wetu wa imani ili ustahimili dhoruba ambazo zitakuja katika kila maisha. Sehemu thabiti muhimu kwa msingi wa imani ni uaminifu wa kibinafsi. Kuchagua kwetu kwa kile kilicho sahihi kila mara wakati chaguzi zimeweka mbele yetu hujenga uwanda thabiti chini ya imani yetu. Inaweza kuanza utotoni kwa vile kila nafsi huzaliwa na kipawa cha bure cha Roho wa Kristo. Kwa yule Roho tunaweza kujua wakati tumefanya kile kilicho sahihi mbele za Mungu na wakati tumefanya kosa mbele Zake. Hizo chaguzi, kwa mamia katika siku nyingi, hutayarisha uwanda thabiti ambao majumba yetu ya imani hujengwa. Vyuma ambavyo dutu ya imani yetu humwagwa ni injili ya Yesu Kristo, pamoja na maagano, maagizo, na kanuni zake zote. Mojawapo ya funguo za imani zinazodumu ni kuhukumu vyema ule wakati wa kukauka unaohitajika. Hii ndio maana nilikuwa mpumbavu kuomba mapema sana katika maisha yangu nipate milima mirefu ya kukwea na majaribu makuu. Huku kukauka hakutokezi kiotomatiki kupitia mpito wa masaa, bali uchukua muda. Kuzeeka peke yake hakutafaa. Ni katika kumtumikia Mungu na wengine daima kwa moyo na nafsi kujufu ambako ubadilisha ushuhuda kuwa nguvu za kiroho zisizovunjika. Sasa, ningependa kuwatia moyo wale waliopo katikati ya majaribu makali, ambao wanahisi kuwa imani yao inafifia chini ya mashambulizi ya shida. Shida zenyewe zinaweza kuwa njia yako ya kuimarisha na hatimaye kupata imani isiyotingisika. Moroni, mwana wa Mormoni katika Kitabu cha Mormoni, alituambia jinsi baraka zinaweza kuja. Anafunza kweli rahisi na tamu kwa kutenda hata kwa kijitawi cha imani humpatia Mungu kuikuza: Na sasa, mimi, Moroni, nitazungumza machache kuhusu vitu hivi; ninataka kuonyesha ulimwengu kwamba imani ni vitu ambavyo vinatumainiwa na havionekani; kwa hivyo, msishindane kwa sababu hamwoni, kwani hamtapata ushahidi wowote mpaka baada ya majaribu ya imani yenu. Kwani ilikuwa kwa imani kwamba Kristo alijionyesha kwa babu zetu, baada ya kuamka kutoka kwa wafu; na hakujionyesha kwao mpaka walipokuwa na imani ndani yake; kwa hivyo, lazima iwe kwamba wengine walikuwa na imani ndani yake, kwani hakujionyesha kwa ulimwengu. Lakini kwa sababu ya imani ya watu amejionyesha kwa watu wa ulimwengu, na kulitukuza jina la Baba, na alitayarisha njia ambayo kwake wengine wangeshiriki kwa mwito wa zawadi ya mbinguni, kwamba wangetumainia vitu hivyo ambavyo hawajaviona. Kwa hivyo, mnaweza kuwa pia na tumaini, na muwe washiriki wa zawadi, ikiwa mtakuwa tu na imani. 7 Ile chembe ya imani iliyo na thamani sana na ambayo unafaa kulinda na kuitumia kwa kiwango chochote uwezacho ni imani katika Bwana Yesu Kristo. Moroni alifunza uwezo wa imani hiyo kwa njia hii: Na wala kwa muda wowote hakujawa na yeyote ambaye amefanya miujiza mpaka awe na imani; kwa hivyo waliamini kwanza katika Mwana wa Mungu. 8 Niliongea na mwanamke ambaye alipokea mwujiza wa nguvu za kutosha ili kuvumilia misiba isiyoweza kufikirika tu kwa uwezo wa kurudia maneno bila kikomo, Najua kwamba Mkombozi wangu yu hai. 9 Imani hiyo na maneno hayo bado yalikuwepo hapo katika ukungu bali hayakufuta kumbukumbu za utotoni wake. Ninashangaa kuona mwanamke mwengine aliyemsamehe mtu 2

aliyemkosea kwa miaka mingi, nilistajabu na kumuuliza kwa nini alichagua kumsamehe na kusahau miaka mingi sasa ya dhuluma. Alisema kwa upole, Kilikuwa kitu kigumu ambacho nimewahi kufanya, lakini nilijua nilifaa kukifanya, Kwa hivyo nilikifanya. Imani yake kwamba Mwokozi atamsamehe kama yeye atawasamehe wengine ilimtayarisha kwa hisia ya amani na matumaini alipokabiliwa na kifo miezi tu baada ya kumsamehe adui wake asiyekuwa tayari kutubu. Aliniuliza, Nitakapofika huko, itakuwaje huko mbinguni? Na mimi nikasema, Mimi najua tu kutokana na kile nimeshaona kuhusu uwezo wako wa kutumia imani na kusamehe kwamba itakuwa makaribisho ya ajabu kwako. Nina tumainisho lingine kwa wale sasa wanaoshangaa kama imani yao katika Yesu Kristo itatosha kwao kuvumilia vyema hadi mwisho. Nimebarikiwa kuwajua wengine wenu ambao mnasikiliza sasa mlipokuwa vijana, wachangamfu, mmezawadiwa kuliko wengi wenu wa karibu nanyi, hali mlichagua kufanya kile Mwokozi angependelea mfanye. Kutoka na wingi wenu mmepata njia za kuwasaidia na kuwatunza wale mnaweza kutowaangalia au kuwadharu kutokana na nafasi zenu katika maisha. Majaribu yanapokuja, imani ya kuyavumilia vyema itakuwepo, iliyojengwa kama mnavyoweza kutambua bali hamkuweza wakati ambao mlitenda juu ya upendo halisi wa Kristo, mkihudumu na kuwasamehe kama vile Mwokozi angefanya. Mnajenga msingi wa imani kutoka kwa kupenda kama vile Mwokozi anavyopenda na kuhudumu kwa ajili Yake. Imani yenu katika Yeye iliwapeleka kwa vitendo vya hisani ambavyo vinaleta matumaini. Bado hajachelewa sana kuimarisha msingi wa imani. Daima kuna wakati. Kwa imani katika Mwokozi, unaweza kutubu na kuomba msamaha. Kuna mtu unaweza kusamehe. Kuna mtu unaweza kushukuru. Kuna mtu unaweza kuhudumia. Unaweza kufanya hivyo popote ulipo na vyovyote unavyohisi mpweke na kutupwa. Siwezi kuahidi kumalizika kwa dhiki yako katika maisha haya. Siwezi kuhakikisha kwamba majaribu yako kuwa yatakuwa ya muda. Mojawapo wa sifa bainifu za majaribu katika maisha ni kuwa yanaonekana kufanya saa kwenda pole pole na kisha karibu kusimama. Kuna sababu za hivyo. Mkijua hizo sababu hazipatiani faraja, bali zinaweza kuwapatia hisia za subira. Hizo sababu zitatokana na jambo hili moja: katika upendo Wao kamili kwako, Baba wa Mbinguni na Mwokozi wanataka ninyi kuunganishwa Nao na kuishi katika familia milele. Ni wale tu watatakaswa kikamilifu kuwa wasafi kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo wanaweza kuwa. Mama yangu alipigana na saratani kwa karibu miaka 10. Matibabu na upasuaji na mwishowe kulazwa kitandani kulikuwa ni kati ya majaribu yake. Nakumbuka baba yangu akisema akimtazama akitweta pumzi zake za mwisho, Msichana mdogo ameenda nyumbani kupumzika. Mmoja wa wanenaji katika mazishi yake alikuwa ni shemejiye na rafiki Rais Spencer W. Kimball. Kati ya kusifia alikofanya, nakumbuka akisema kitu kilichokuwa kama hiki: Wengine wenu mnaweza kufikiria kwamba Mildred aliteseka kwa muda mrefu na sana kwa sababu ya kitu alifanya makosa ambacho kilihitaji majaribu haya. Kisha akasema, La, ni kwamba Mungu alitaka kumkwatua kidogo zaidi. Nakumbuka wakati huu nikifikiria, Kama wanamke mwema hivi alihitaji kukwatuliwa zaidi, basi ni nini kilichokuwa kinaningoja mimi? Kama tuna imani katika Yesu Kristo, nyakati zile ngumu na zile rahisi katika maisha zinaweza kuwa baraka. Katika hali zote, tunaweza kuchagua kilicho sahihi kwa mwongozo wa Roho. Tuna injili ya Yesu Kristo kuchonga na kuongoza maisha yetu kama tutachagua hivyo. Na manabii wakifunua kwetu nafasi zetu katika mpango wa wokovu tunaweza kuishi kwa matumaini kamili na hisia za amani. Hatutakuwa na haja ya kuhisi kwamba tu wapweke au hatupendwi katika huduma ya Bwana, kwa sababu sivyo kamwe. Tunaweza kuhisi upendo wa Mungu. Mwokozi ameahidi malaika kushoto kwetu na kulia kwetu, atatuhimili. 10 na Yeye hutimiza neno Lake. Nashuhudia kwamba Mungu Baba yu hai na kwamba Mwanawe Mpendwa ni Mkombozi wetu. Roho Mtakatifu amethibitisha kweli katika mkutano huu na atafanya hivyo tena kama mtatafuta kama mnaposikiliza na mnaposoma hapo baadaye jumbe za watumishi wa Bwana wenye mamlaka ambao wako hapa. Rais Thomas S. Monson ni nabii wa Bwana kwa ulimwengu wote. Bwana anawalinda. Mungu Baba yu hai. Mwanawe Mpendwa, Yesu Kristo, ndiye Mkombozi wetu. Na upendo Wake upo daima. Nashuhudia hivi katika jina la Yesu Kristo, amina. MUHTASARI 1. Spencer W. Kimball, Give Me This Mountain, Ensign, Nov. 1979, 79 2. Mafundisho na Maagano 122:7 9. 3. Mafundisho na Maagano 19:15 19. 4. Yeremia 46. 5. Yoshua 1:5. 6. Ona Thomas S. Monson, Look to God and Live, Ensign, May 1998, 52 53. 7. Ether 12:6 9. 8. Ether 12:18. 9. Ona I Know That My Redeemer Lives, Hymns, no. 136. 10. Ona Mafundisho na Maagano 84:88. 2012 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa. Imechapishwa USA. Kiingereza kiliidhinishwa: 6/11. Tafsiri iliidhinishwa: 6/11. Tafsiri ya Visiting Teaching Message, May 2012. Swahili. 10365 743 3