KANISA LINAHITAJI KUJUA

Size: px
Start display at page:

Download "KANISA LINAHITAJI KUJUA"

Transcription

1 Miki Hardy KANISA LINAHITAJI KUJUA Umefika wakati tuyazungumzie mambo kadhaa ya msingi waziwazi ili Wakristo watambue ya kwamba Bwana ana mambo mazuri zaidi kwa ajili yao!

2 Hakimiliki 2013 na Church Team Ministries International (CTMI) Kanisa Linahitaji Kujua na Miki Hardy. Imechapishwa na Church Team Ministries International (CTMI) Toleo la kwanza: Julai 2015 Jalada limebuniwa na: Idara ya Habari ya CTMI Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu ya chapisho hili inayoweza kunakiliwa, kusambazwa,au kutolewa kwa namna yo yote ile isipokuwa kwa ruhusa ya mchapishaji. Vifungu vya Biblia vimetolewa katika Biblia, Swahili Union Version, Machapisho mengi ya Church Team Ministries International yanapatikana kwa gharama nafuu ikiwa yananunuliwa kwa jumla kwa ajili ya kutangaza, kuchangisha fedha, kugawa bure, na kwa kuelimishia. Kwa maelezo zaidi, tuandikie: Media Dept., CTMI, Trianon, Mauritius; au tuma baruapepe kwa: Tembelea tovuti yetu: ISBN

3 Yaliyomo I. Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka... 5 II. Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? III. Mkristo na Pesa IV. Mungu na Muziki V. Vita ya Rohoni VI. Mahusiano Kabla ya Ndoa VII. Barabara ni Nyembamba VIII. Kanisa Litakabiliwa IX. Yesu Anaita Tena

4 4

5 Sura ya I Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka 5

6 Wakristo wengi leo wanaweza kukumbuka wakati ambapo suala la talaka kwa mchungaji au kiongozi wa Kanisa lilikuwa ni jambo la aibu isiyoneneka. Hapakuwepo na uwezekano kwa mtu wa jinsi hiyo kuendelea katika utumishi. Zaidi na zaidi, leo tunaona wachungaji wakitoa talaka, wakioa upya na kuendelea na huduma kana kwamba hakuna jambo zito lililofanyika. Ninaamini haya ni matokeo ya anguko na udini ambavyo vimechukua nafasi ya fundisho la uzima na Kweli ya Kibiblia ndani ya Kanisa. Hili ndilo chimbuko la hii hali ya mambo. Sasa, ikiwa mchungaji anaweza kumpa mkewe talaka na akaendelea kuwaongoza watu wa Mungu, je! waumini wanapata mfano wa jinsi gani wa kuiga? Labda maswali tunayopaswa kujiuliza ni, Ni kwa nini Wakristo wawili waliojazwa Roho Mtakatifu washindwe kutatua tofauti zao na, Je! kuna uhalali wo wote kwa haya matatizo kutotatulika, au kwa wawili hawa kuachana? Ama liwe linamhusu mchungaji, au mshirika wa kanisa, ninaamini suala la kutengana, kutoa talaka, na kufunga ndoa mara ya pili hufanyika kwa sababu hawa watu hawajui wajibu wao kamili mmoja kwa mwingine katika ndoa. Tunaona kwenye Maandiko ya kuwa mume ana wajibu mkubwa mno: kumpenda mkewe kama Kristo anavyolipenda Kanisa. Vivyo hivyo, mke naye ameitwa amtii mumewe. Kama wawili hawa wasipouchukua msalaba wao, na kumruhusu Roho wa Mungu awavunje na kuwabadilisha, hilo kamwe halitakuja kutokea Mungu peke yake ndiye anayeweza kulifanya hili mioyoni mwao. Hakuna mbinu inayoweza kulifanya hili ni matokeo ya kazi ya Msalaba maishani mwao! 6

7 Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka Sijaona popote kwenye Maandiko kinachonielekeza kuamini ya kuwa ni mapenzi ya Mungu kwa wanandoa Wakristo, achilia mbali mchungaji, kutoa talaka. Hii ni kwa sababu Mungu, kwa njia ya Msalaba, ameleta njia ya kurejesha upendo na umoja kati yao. Hebu sasa tuangalie Neno la Mungu linavyotufunulia kuhusu suala la ndoa na talaka Siku hizi, watu wengi hawaoni shida kwa Wakristo wanandoa kuachana kwa sababu tu mmoja wao hapatani na mwenzake; au kwa kuwa tu hawana mtazamo mmoja kuhusu mambo mbalimbali au hawana tena maono mamoja! Hakika hili ni eneo ambalo Kanisa limekubali kuathiriwa si tu na njia za ulimwengu usioamini, bali pia na viongozi wa Kikristo ambao wameandika vitabu, wakihalalisha matendo yao ya kibinafsi sana na ambao, kwa kuamua kuchukua njia ya talaka wamefungua mlango kwa waumini kufanya vile vile. Ninaamini ya kwamba badala yake, tunapaswa tuuangalie mtazamo wa Mungu juu ya suala hili. Ndoa Kwenye Agano Jipya Kwenye kitabu cha Mwanzo, Mungu aliianzisha ndoa. Baada ya yale Yesu aliyokamilisha Msalabani, ndoa ya kwenye Agano la Kale, yenye wake wengi na hati za talaka, haiwezi tena kulinganishwa na ndoa chini ya Agano Jipya. 7

8 Mpango wa Mungu kwetu sisi, kama Wakristo tuliozaliwa mara ya pili, ni kuishi na waume zetu na wake zetu hadi kifo kitakapotutenganisha. Katika Marko 10:2, kwa kuwa Yesu alikuwa akiwahoji Mafarisayo juu ya mtazamo wao wa kisheria katika masuala mengi, walimjaribu kwa kumwuuliza: Je, ni halali kwa mtu kumwacha mkewe? Yesu akawaonyesha ya kuwa, chini ya Musa na Torati, Mungu aliruhusu talaka kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao (Marko 10:5); lakini katika Agano Jipya, mambo yangekuwa tofauti. Katika Mathayo 5:32, anazungumzia waziwazi juu ya kile kinachotarajiwa kwa waamini wote wa Agano Jipya: Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini. Isipokuwa kwa habari ya uasherati bila shaka haimaanishi pale mwenzi mmoja anapoanguka katika dhambi na kufanya tendo moja la uasherati au la kukosa uaminifu. Inazungumzia mtu ambaye amerudi nyuma na anaishi katika dhambi, na aliyedhamiria kuendelea kuishi katika dhambi. Kwa kuiruhusu talaka katika mazingira hayo maalum, Yesu hajaondoa ukweli kwamba yule aliyekosewa bado anatakiwa kunyenyekea na kusamehe. Hili linaweza kufanyika kwa dhati pale tu tunapoikubali njia ya Msalaba. Kwa hivyo, Biblia iko wazi: kwenye Agano Jipya, hakuna uhalali wowote wa kutoa talaka isipokuwa katika maeneo maalum sana vinginevyo itapunguza kile Yesu alichokifanya Kalvari! 8

9 Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka Injili Zisizokuwa Na Uweza Nina hakika utakuwa umegundua ya kuwa Kanisa limepoteza mwelekeo katika hili eneo, na linaenenda kama vile Injili ni kitu kinachobadilika kwa kutegemea nyakati. Katika miongo michache iliyopita, Kanisa, kwa kujumuisha wachungaji na viongozi, kwa usahihi kabisa, halikukubaliana na talaka, lakini leo hii talaka imekubalika makanisani. Ni nini kilichofanyika? Bila shaka ni kwa sababu injili inayohubiriwa leo hii imebadilika na haina uwezo wa kushughulika na mambo ya jinsi hiyo. Haina nguvu tena ya kuihakiki dhambi kama mwanzoni. Mfano mzuri ni injili ya Mafanikio inayovuta mioyo ya watu kuyaandamia mambo ya mwilini badala ya kutafuta makuzi ya rohoni. Haijengi, na hakika haina uwezo wa kukabiliana na mambo ya ndani ambayo Wakristo wanapambana nayo leo. Hii ndio maana ni muhimu turejee kwenye injili ya ufunuo wa Msalaba ikiwa tutataka kuona familia za Kikristo zenye umoja pamoja na kupungua kwa kiwango cha talaka Kanisani. Siku hizi Wakristo mara nyingi wanataka njia rahisi ya kutatua matatizo yao ya ndoa, mlango rahisi wa kutokea. Wanaachana kwa sababu nyepesi kama vile: Mke wangu hanitii ; Mume wangu si mtu wa rohoni, au mbaya zaidi, Hatupatani tena, maono yetu na matarajio yetu yamebadilika Watu wa jinsi hii bila shaka hawajaisikia injili sahihi, kwani injili sahihi itawaongoza katika kuwajibika kila mmoja kwa mwenzake. 9

10 Nafasi Ya Mume Niruhusu nifafanue juu ya ufunuo wa ajabu Paulo aliopewa kuhusu ndoa kwenye Waefeso 5. Uhusiano wa mume na mke ndio tu uliolinganishwa katika Agano Jipya na uhusiano Yesu alio nao na Kanisa lake. Paulo anatamka kwa ujasiri ya kuwa, KAMA Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake VIVYO HIVYO mume naye anapaswa kumpenda mke wake. Yesu alijinyenyekeza, akachukua sura ya mwanadamu, akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Hiyo ndiyo hali ya moyo Yesu anayoagiza mume awe nayo kwa mke wake. Huo ndio wajibu wa mume: kama Yesu, yeye naye anaitwa apoteze haki zake na autoe uhai wake kwa ajili ya mke wake. Huu ndio ufunguo wa ndoa yenye mafanikio. Utaratibu Wa Mungu Kwenye Ndoa Nafasi ya mke imefananishwa na ile ya Kanisa. Paulo anatamka ya kuwa KAMA vile Kanisa limtiivyo Kristo, VIVYO HIVYO mke naye anapaswa kumtii mumewe. Kwa hivyo, Kanisa wewe na mimi linapoelewa kile Yesu alichofanya msalabani kwa ajili yetu; kwa maneno mengine, upendo aliouonyesha, sisi nasi tunaweza kumpenda pia. Isingewezekana tumpende Yeye kabla ya kuujua upendo wake kwetu. Je, unaweza ukaona utaratibu wa mambo hapa? 10

11 Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka Ni wazi, basi, kwamba mume ana wajibu mkubwa zaidi kuliko mke katika ndoa, kwani huduma yake inalinganishwa na ya Kristo, ilhali ya mke imefananishwa na ya Kanisa. Ikiwa mume atakuwa tayari kuchukua hatua ya kwanza, katika kuutii wito wake, kama Kristo alivyofanya, moja kwa moja atavuna hali ya utii kutoka kwa mke wake. Katika mazingira ya kawaida, hatutarajii kwamba utii wa mwanamke kwa mumewe utakuwa wa moja kwa moja; lakini msingi sahihi unapokuwepo, mume anaweza akatarajia ya kuwa mkewe atamnyenyekea. Hata hivyo, hata kama mke hatafanya vile, mume anapaswa aendelee kuyatoa maisha yake kwake, na amtegemee Mungu kufanya muujiza moyoni mwa mkewe. Mwishoni mwa kifungu hiki, Paulo ananukuu andiko kutoka katika Agano la Kale, Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Moyo wa Mungu kwa ajili ya ndoa ni mume na mke wadumu katika umoja maisha yao yote. Tunapozitii amri za Mungu, yeye ni mwaminifu na hutenda miujiza. Mume Wa Mke Mmoja Yapo mambo mengi sana yahusuyo ndoa ambayo hayajatajwa katika Biblia. Kanisani mwetu penyewe tumeshuhudia matukio mengi tofauti katika miaka hii mingi, na tumejifunza kuyatatua kila moja kwa namna yake, katika neema na kweli. Mahali ndugu wa kiume au wa kike alipoichukua njia ya Msalaba, na kuiruhusu toba kufanya kazi 11

12 moyoni mwake, tumeshuhudia urejesho na ushindi maishani mwao na katika utumishi wao kwa Bwana. Na hebu niongeze kusema ya kwamba Mungu si Mungu anayetoa nafasi ya pili au ya tatu ya kujaribisha mambo. Mpango wake sikuzote ni kwa mume kuwa na mke mmoja, na ametuwezesha katika hilo kwa kumtuma Yesu katika mfano wa mwanadamu, afe Msalabani na kuishinda dhambi katika mwili. Ni juu yetu kuyatoa maisha yetu yawe dhabihu ili miili yetu isulubiwe. Mwanamume anayemwacha mkewe halafu akaendelea katika utumishi kana kwamba hakuna kilichofanyika, hawezi kutarajia kuendelea kubeba upako ule ule katika utumishi wake kwa Bwana, na hasa ikiwa ameoa tena, hadi atakapoacha kuhalalisha uamuzi wake huo na kutubu. Ufunguo Unaoleta Matengenezo Si mpango wa Mungu kwa mtu yeyote kumwacha mwenzi wake. Mungu anachukia talaka; lakini hawakatai wale walioachana au waliooa ama kuolewa mara ya pili ikiwa watatubu. Ikiwa nimegusa eneo linalokuhusu, hujachelewa. Mungu anaweza kukurejesha, pamoja na utumishi wako kama uko kwenye huduma, ikiwa utakuwa tayari kukiri ya kuwa haukuenenda sawasawa na moyo wala Neno la Mungu, bali ulifuata tamaa za mwili wako; na ya kuwa, inawezekana ulijiingiza katika mahusiano yasiyo sahihi. 12

13 Sura ya I - Moyo wa Mungu Juu ya Ndoa na Talaka Ikiwa ni hivyo, ni lazima umrudie Bwana kwa toba ya kweli; kulingana na maongozi ya Roho Mtakatifu, na ukiwa na utayari wa kufanya lolote atakalokuagiza kufanya... hata kama itakulazimu kumrudia mwenzi wako wa mwanzo. Kumbuka ya kwamba Bwana hahitaji sababu au maelezo kuhusu mwenzi wako, au kuhusu yale aliyoyafanya. Yeye huuangalia moyo wa mtu. Katika kila jambo, Mungu anatamani tuwe na moyo safi, mnyenyekevu, uliojaa msamaha, na ulio na toba. Inawezekana yakawepo mahusiano ambayo pengine hayawezi kurekebishika; ila, mengi zaidi yanarekebishika, ikiwa tuko tayari kujikana nafsi zetu na kuuchukua msalaba wetu. Msalaba ndilo suluhisho la Mungu kwa ndoa yenye mafanikio! 13

14 14

15 Sura ya II Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? 15

16 Katika safari zangu barani Afrika katika miaka 25 iliyopita, swali moja limekuwa likijitokeza mara kwa mara: Je, inawezekana kwa Mkristo aliyezaliwa mara ya pili kupagawa mapepo? Hili jambo mara nyingi huhusishwa na maisha aliyoishi mhusika huko nyuma, au kibaya zaidi, linahusishwa na mambo waliyoyafanya mababu zake. Inanihuzunisha kuona kwamba kuna Wakristo wengi wanaoamini ya kwamba wao, au ndugu zao wa kiume na wa kike katika Kristo wanaweza kupagawa mapepo baada ya kupokea wokovu. Sote tunakubali ya kuwa kazi za mapepo na roho chafu zipo. Lakini je! inawezekana kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kuhitaji kufunguliwa kutokana na nguvu za mapepo? Ninaposoma Maandiko, jibu langu kwa swali hili ni Hapana! yenye nguvu. Biblia iko wazi kuhusu hili suala: tunapozaliwa mara ya pili, tunaokolewa kutoka katika nguvu za giza na kuingizwa katika Ufalme wa Yesu Kristo. Roho Mtakatifu anakuja kuishi ndani yetu na nuru haiwezi kukaa pamoja na giza. Hakuna jinsi kabisa ambapo pepo anaweza akaishi ki-kwelikweli ndani ya Mkristo aliyezaliwa mara ya pili, aliyeyatoa maisha yake kwa Bwana Yesu Kristo na anayetamani kumtumikia. Haiwezekani kabisa! Tunapaswa tuhoji wokovu wa watu waliojitokeza kwenye mikutano na kuungama sala ya toba, halafu wakaendelea kudhihirisha dalili za kupagawa mapepo. Katika hali kama hizo, labda tungepaswa kuuliza swali: Je, toba ya kweli imefanyika mioyoni mwao? Lakini cha muhimu zaidi, ni kwamba ninaamini matatizo mengi yanayosingiziwa pepo ni madhihirisho tu ya mwili. Kwa bahati mbaya, 16

17 Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? Wakristo wengi wameaminishwa ya kwamba haya madhihirisho ya mwili ni kazi za Shetani. Jambo ambalo Kanisa linapaswa kujua ni kwamba, katika hali kama hizi, maombezi ya ukombozi sio jawabu. Maisha yetu yanapooana na mfano wa Yesu Kristo, na tunapouchukua Msalaba wetu kila siku, na kuifisha miili yetu na kumfuata yeye, suala la kupagawa pepo halitakuwa tatizo maishani mwetu, au kwa Kanisa. Ulimwengu wa roho upo na unaweza kuwa na nguvu kuliko tunavyofikiri. Ndio maana Mungu anapogusa maisha yetu tunaweza kubadilishwa mara moja. Kwa msingi huo huo kuna watu ambao maisha yao yameathiriwa na mapepo pamoja na roho za kishetani. Katika vitabu vya injili, Yesu mwenyewe alitoa pepo na kuwaweka watu huru. Ukweli kwamba watu wanapagawa mapepo upo na hauwezi kupingwa. Hata hivyo, katika Mathayo 12, Yesu anapozungumza juu ya kutoa pepo, alizungumza kabla ya Msalaba na alikuwa akizungumzia kizazi kikaidi, sio Kanisa. Kwa hivyo, swali langu ni hili: Wakristo waliozaliwa mara ya pili, waliotubu dhambi zao za kale, na kuyasalimisha maisha yao kwa Yesu, je! bado wanahitaji kufunguliwa kutoka katika nguvu za mapepo? Kuzaliwa Mara Ya Pili Au Kutokuzaliwa Kabisa Sijaona mahali popote kwenye Biblia Wakristo katika Kanisa la mwanzo wakitolewa mapepo. Ama umezaliwa mara ya pili au la; 17

18 hakuna zaidi! Kabla ya kumjua Yesu tulikuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Hatukumjua Mungu; na sisi sote pia tulikuwa chini ya ushawishi wa roho za kishetani au tulitawaliwa nazo (Waefeso 2:1-5). Mtu asiyeamini anapotubu dhambi zake na kuamini katika dhabihu ya Yesu msalabani, Mwenyezi Mungu mwenyewe huja na kuishi moyoni mwake. Wakolosai 1:13 inaelezea hivi: Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake. Baada ya sisi kuzaliwa upya na Roho Mtakatifu, asili ya Mungu inachukua nafasi ya asili ya dhambi iliyotutawala mioyoni mwetu hapo kabla. Mara nyingi sio lazima hata kuomba ili mtu afunguliwe. Yule asiyeamini tayari yuko chini ya hukumu kubwa sana na yuko tayari kuyasalimisha maisha yake kwa Kristo, kiasi kwamba anawekwa huru kwa wepesi sana kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Mara nyingine anahitajika kufanyiwa maombi ili afunguliwe. Kutokana na hayo unaweza ukauliza je, maana yake nini haya madhihirisho ya nguvu za giza leo hii makanisani? Jawabu ni kwamba watu wengi huja tu kwa ajili ya kupokea uponyaji na kufunguliwa kutokana na nguvu za giza, kubarikiwa, na si kumtafuta Mungu kwanza. Na kwa sababu hawajazaliwa mara ya pili, nguvu za giza huendelea kuyatawala maisha yao. Lakini haiwezekani kwa Wakristo waliozaliwa mara ya pili kuendelea kuwa chini ya nguvu za mapepo, isipokuwa wamerudi nyuma hadi kuvunja kabisa uhusiano wao na Kristo, wamemkataa Bwana na kuzifungulia mlango kazi za mapepo mioyoni mwao na 18

19 Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? maishani mwao. Kwa sababu, inawezekanaje Roho Mtakatifu kuishi kwenye mwili mmoja na pepo? Shida nyingi na mambo mengi yanayohusishwa na mapepo yana mizizi yake kwingineko. Kama hatupo kwenye msingi wa Msalaba tunajikuta tukipokea kila aina ya mafundisho ya uongo na imani za kigeni. Kwa kila jambo linaloharibika tunatupia pepo lawama. Ni Mwili! Ni lazima ieleweke kwamba ikiwa mimi kama Mkristo nina shida na mwili wangu, haina maana kwamba kuna pepo ndani yangu ila ni kwamba tu nimeziruhusu tamaa za mwili wangu zinitawale. Ni kweli twaweza kujaribiwa, lakini ni lazima tutofautishe kati ya kujaribiwa na kumilikiwa na roho chafu. Ni pale tu nitakapojikana nafsi yangu, kuwa tayari kuziachilia haki zangu na kuyapoteza maisha yangu kwa kuuchukua msalaba wangu, ndipo nitakapopata ushindi katika eneo husika. Sihitaji kabisa kukemewa pepo yeyote atoke, maana tayari niko huru na mapepo! 19

20 Maombi ya Kufunguliwa Sio Jawabu Mungu ametufungulia njia ya kutokushindwa na miili yetu, au kuzisikiliza tamaa zake. Ni Msalaba. Ndio maana maisha yetu hayana uhusiano wowote na mapepo. Roho wa Mungu anaishi ndani yetu. Yeye anatuombea na kutuwezesha, kwa neema ya Mungu, kuusulubisha huu mwili. Kile Mungu anachotaka kufanya maishani mwako kwa njia ya utakaso hakiwezi kupatikana kupitia maombezi ya kutoa pepo. Usimruhusu mtu yeyote ajaribu kukemea ndani yako pepo wa hasira, uvivu, wivu na kadhalika. Vivyo hivyo huwezi kutatua tofauti zilizopo kati yako na mwenzi wako, watoto wako au Mkristo mwenzako kwa kukemewa pepo... Haya ni madhihirisho ya mwili wako, matokeo ya maisha ambayo hayajasalimishwa kwa Bwana. Wakristo wengi leo wamekata tamaa kwa sababu wanafahamu ni aina gani ya watu wanaopaswa kuwa, lakini wanapoitazama hali halisi ya maisha yao, wanahisi tu kushindwa na kukata tamaa. Hivyo wanakimbilia kwenye kutolewa pepo. Ushindi upo katika Msalaba. Hebu kuwa na utayari wa kuyapoteza maisha yako na utaona matokeo yake... Tunaweza kuwa dhaifu katika maeneo mengi, lakini bado tukaudhihirisha uzima wa Kristo. Tumewekwa huru mbali na mapepo na tunaitembelea hiyo njia ya kuuelekea ukamilifu; Bwana apewe sifa! Kwa maelezo kuhusiana na kazi za mwili, angalia orodha iliyoko Wagalatia 5: Na hebu nikuambie, huhitaji kutolewa pepo ili uweze kutembea katika ushindi dhidi ya mambo haya. Chukua tu msalaba wako. 20

21 Sura ya II - Je, Wakristo Wanaweza Kupagawa Mapepo? Kujifananisha Na Kristo Ni muhimu tuweze kuelewa kusudi la ujumbe wa Msalaba kwa maisha yetu. Ni lazima tuwe tayari kujifananisha na mauti ya Kristo ili tuweze kuubeba uzima wake na kuwa huru. Mara tu tunapouweka msalaba kando, tunatafuta njia za mkato, au jambo mbadala kama vile kukemewa pepo, yaani, aina ya Ukristo wa kubonyeza kitufe. Lakini katika Wagalatia 2:20, maneno ya Paulo, Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu ni tamko la ajabu linalodhihirisha aina ya maisha aliyoishi. Kupitia ufunuo alioupokea, Paulo alijifunza ya kwamba alihitajika ayafananishe maisha yake na maisha ya Kristo, ajikane nafsi yake, ausulubishe mwili wake. Aliuishi huo ufunuo na akaweza kuuhubiri; maisha yake yalikuwa ni ushuhuda wa mabadiliko yanayoletwa na kazi ya Msalaba. Ujumbe wa Msalaba ni onyo la mara kwa mara na kumbukumbu inayoufunua udhaifu wa miili yetu, na kutuwezesha kuona hali halisi ya maisha yetu. Inatuleta kwenye toba, kujikana nafsi na kurejea Msalabani. 21

22 Huru Kweli Kweli! Kwa hivyo, ndugu au dada mpendwa, ikiwa kutoka katika vina vya moyo wako umeyasalimisha maisha yako kwa Kristo, tofautisha kati ya udhaifu wa mwili wako na kupagawa mapepo. Unaweza ukawa ni Mkristo dhaifu, ila tambua umewekwa huru mbali na mapepo. Haleluya! Ndio sababu Mtume Paulo alinena sana juu ya hatari za mwili. Alifahamu fika udhaifu wa mwili. Kumbuka, Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli! 22

23 Sura ya III Mkristo na Pesa 23

24 Kama kuna eneo ambalo Wakristo leo hii wamelaghaiwa na kufundishwa mafundisho yenye udanganyifu, hakika ni katika eneo la fedha na utoaji. Ni aibu kubwa kwa Kanisa kuona wachungaji wengi wakilikosesha kundi la Mungu kwa kuwapa ahadi za uongo za mafanikio na baraka; wakiwapotosha kwa kutumia sheria zinazowashurutisha kutoa. Mara nyingi nimelishutumu fundisho la mafanikio lililolivamia Kanisa, kwenye nchi tajiri na nchi maskini. Jumbe zangu zimeelezewa kuwa zenye utata kwa sababu nimepinga kuhubiriwa fundisho hili la uongo. Sina tatizo kabisa Wakristo wanapotajirika kwa mali za ulimwengu huu, na wanapobarikiwa. Lakini ninapingana vikali na mafundisho ya kwamba ni mapenzi ya Mungu ya kuwa Wakristo wote wameitwa kuwa matajiri. Hili linapatikana wapi kwenye Biblia? Hata Kanisa la Mwanzo lilikuwa na Wakristo maskini. Kwa hivyo, ninaamini ni uzushi kuwaaminisha Wakristo wote ya kwamba ni mapenzi ya Mungu wote wawe matajiri, wote wamiliki majumba makubwa, magari ya kifahari, n.k., au ya kwamba wanapoendelea kubaki maskini ni kwa sababu hawana imani uzushi kabisa! Katika maeneo kama Afrika na India, Wakristo wengi wanaishi katika umaskini wa kutisha. Hakuna aibu katika hilo, na haimaanishi hawana imani. Zaidi ya hilo, katika mahubiri mengi ya siku hizi, pesa inapewa umuhimu kupita kiasi! 24

25 Sura ya III - Mkristo na Pesa Si kwamba ninalishambulia fundisho la mafanikio, lakini ninaamini tunahitajika tuangalie Neno la Mungu kuhusu hili suala katika mtazamo sahihi katika kuutafuta moyo wa Mungu kwa hili. Kinachonisikitisha zaidi ni kwamba waumini katika makanisa ambapo injili ya jinsi hii inahubiriwa, na ambao wengi wao ni maskini, hawafiki mahali pa kuelewa ya kwamba Mungu ana haja na aina ya moyo tulionao katika kumtolea. Mungu humpenda mtu anayetoa kwa moyo mkunjufu, si mtoaji tajiri! Katika makanisa mengi sana, linapokuja suala la utoaji, watu wanaleta sadaka zao wakitaraji kurudishiwa kwa wingi walichopanda, au kutokana na shinikizo na hofu ya kuonekana wanaenda kinyume na kile Biblia inachosema! Ila, tunapolitazama Neno la Mungu, je! ni wapi tunapomuona Yesu au Mitume wakizungumzia mafanikio kwa mtazamo wa jinsi hii? Jambo lililo wazi ni kwamba Mungu ameahidi kuyashughulikia maisha yetu (Mathayo 6:25-26); ni udhihirisho wa moyo wa Mungu kwa watu wake na maono yake kwa ajili ya Ufalme. Biblia sio kitabu chenye mbinu na kanuni kwa wahubiri kutumia ili kuwaomba ninyi muwape pesa ili Mungu aweze kuwabariki. 25

26 Kumpenda Yesu, Kuupenda Ufalme Wake Mpango wa Mungu kwa Kanisa lake ni kwamba Wakristo wabebe moyo wake uwe ushuhuda kwa ulimwengu usioamini. Kwa Mkristo mwenye shukrani anayejua kuwa Yesu alitoa kila kitu kwa ajili yake, ambaye moyo wake unamilikiwa na Mungu na ambaye maisha yake yamebadilishwa na Kristo, kutamani kumtolea Mungu ni asili yake. Si mtu anayeleta matoleo yake kwa sababu analazimika kufanya hivyo, au kwa sababu mtu fulani amemwambia atoe kiasi fulani, au kwa kuwa amefundishwa jinsi ya kumtolea Mungu. Na hakika hatoi ili abarikiwe. Anatoa kwa sababu anampenda Yesu na Ufalme wa Mungu; ana shukrani kwa ajili ya wokovu. Maisha yake yamefananishwa kikamilifu na ya Kristo, na moyo wake umetolewa kikamilifu katika kuyatumikia maono ya Mungu kwa Kanisa lake. Hapa yupo mtu mwenye uwezo wa kutoa vyote, juu sana kuliko asilimia yoyote iliyopangwa au kiwango chochote kilichowekwa. Yeye hupanda kwa furaha katika Ufalme wa Mungu kwa kadiri anavyoongozwa na Roho Mtakatifu. Mkristo wa aina hii anaweza kutoa kwa ukarimu hata katika nyakati za uhitaji mkubwa, kama tunavyoona Kanisa la Makedonia likifanya katika 2 Wakorintho 8. Anatenda huku akiamini ya kuwa Mungu atashughulikia mahitaji yake binafsi, kwa sababu anajua moyo wake ni kwa ajili ya Ufalme. 26

27 Sura ya III - Mkristo na Pesa Mungu Anataka Tufanikiwe Kuna vifungu viwili vya Maandiko ambavyo karibu kila Mkristo anavijua; kwani, katika nyakati fulani, wengi wetu huenda tumesikia vikifundishwa kuhusiana na utoaji na mafanikio. Katika maeneo yote mawili, mafundisho ya uongo yamepenyezwa Kanisani ikiwa ni matokeo ya wahubiri kuichukua mistari hii kwa maana nyingine Katika 3 Yohana 1-8 tunasoma, Mpenzi, naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo. Sote tunafahamu kuwa Mtume Yohana anamsifu Gayo kwa moyo, upendo, jinsi anavyoujali Ufalme, na ukarimu wake kwa watu wa Mungu. Je, si ni jambo la kawaida kabisa kwa Yohana kumtaka Mungu ambariki mtu wa jinsi hii? Mtume anataka Gayo afanikiwe katika mambo yake yote, kwa sababu anajua chochote anachopewa na Bwana kitatumika kuwabariki ndugu wengine na kitakuwa na manufaa katika Ufalme. Sasa, tunarukaje kutoka kwenye kweli hii hadi kutangaza kuwa ni mapenzi ya Mungu - ni kusudi lake na mpango wake - kwamba Wakristo wote wafanikiwe kifedha; kwamba Wakristo wote wanapaswa watarajie kupokea mara mia kama malipo, endapo watatoa kwa ajili ya mhubiri huyu au mradi ule? Hili ni kinyume na Maandiko! Tunachoweza kusema bila shaka yo yote ni kwamba Mungu angependa kumbariki kila Mkristo, ambaye, kama Gayo, ana moyo kwa ajili ya Ufalme, na ni mkarimu kwa watu wa Mungu. 27

28 Maono Ya Agano Jipya Tunaposoma maneno ya Yesu katika Luka 6, tunaona roho ile ile na moyo ule ule aliokuwa nao Yohana na mitume wengine wote. Hapa (mistari 27-46) Yesu anazungumza na makutano kuhusu kuwa na moyo mwingine na maono mengine... moyo na maono ya Ufalme. Anawasihi watu kutoa maisha yao na kumruhusu Mungu awabadilishe ili waishi sawasawa na Agano Jipya. Kwamba, katika mtazamo huu anasema katika msitari wa 38: Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa, si sababu ya mtu kutafsiri kuwa alikuwa akizungumzia utoaji na mafanikio. Hiki kifungu kinahusu aina ya moyo anaopaswa kuwa nao Mkristo ambaye daima anashughulishwa na Ufalme wa Mungu. Kwa msingi huo Yesu anamalizia, katika msitari wa 46 kwa kusema, Na kwa nini mnaniita Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? Kwa hiyo, hapaswi mtu yeyote kutumia andiko hilo kushawishi watu ya kuwa wakitoa, bila kujali hali za mioyo yao au nia wanayotoa nayo, ya kwamba Mungu bado anawajibika kuwabariki. Hii ndiyo maana leo hii kuna mamilioni ya Wakristo ambao bado wanasubiri baraka zao! 28

29 Sura ya III - Mkristo na Pesa Kwa Kadri Ya Uhuru Wa Moyo Wako Niruhusu niseme ya kwamba ikiwa bado unaamini kuwa unalazimika kumtolea Mungu, hujaelewa undani wa kile ambacho Yesu Kristo alifanya pale msalabani; ukombozi aliotupatia Mwana wa Mungu. Ametuweka huru. Leo hii tuko huru kutoa kutoka katika ndani ya mioyo yetu, kwa kadiri tunavyoongozwa na Roho Mtakatifu. Je, unafahamu ya kuwa kama nitamtegemea mtu au sheria yoyote katika Agano la Kale iliyo chini ya ukuhani wa ki-lawi kuniambia ni kiasi gani ninachotakiwa kutoa, ninaweza nikajikuta nikitoa chini zaidi ya kiwango nilichodhamiria moyoni kutoa? Sasa katika mtazamo halisi tunaona moyo wa Mkristo wa Agano Jipya katika tamko la Mtume Paulo katika 2 Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. Hapa hatuoni Mkristo mwenye hofu, na mnyimivu, anayelazimika kutoa kwa sababu anawajibika kutoa, au kwa sababu kila mtu atafahamu kiasi alichotoa. Kutumika Katika Uhuru Makanisa ya Makedonia yalikuwa na uwezo wa kutoa licha ya umaskini wao mkubwa, ikiwa ni matokeo ya Injili iliyowafanya kukubali 29

30 kupoteza maisha yao, kujikana nafsi zao, kuuchukua msalaba kila siku na kumfuata Yesu. Ukarimu wao ulikuwa ni matunda ya kazi ya injili, si matokeo ya kulaghaiwa kihisia. Walitamani kutoa kutoka katika vina vya mioyo yao, na wakasisitiza kutaka kushiriki katika mradi wa kiroho na wenye manufaa kwa Ufalme na kwa watakatifu wengine. Tafadhali elewa kuwa sitaki kukufanya uangalie nyuma na uanze kuhoji ni kwa jinsi gani au ni kwa lipi ulilotolea pesa zako huko nyuma. Lakini ninaamini kuna Wakristo wengi wanaotafuta kuujua ukweli. Nami ninachotaka ni kwa Kanisa kuujua moyo wa Mungu kwenye suala la pesa; fundisho la kweli ni lipi kulingana na Neno lake ili, kwa neema yake na kwa kuongozwa na Roho wake Mtakatifu, tuweze kuwa huru kumtumikia Mungu kwa pesa zetu. 30

31 Sura ya IV Mungu na Muziki 31

32 Sitakuwa ninatia chumvi nikisema ya kwamba uzi unaotenganisha muziki wa kidunia na kile kinachoitwa Muziki wa Kikristo wa Kizazi Kipya, ni mwembamba kwelikweli. Inasikitisha, lakini uimbaji mwingi tunaousikia Kanisani siku hizi ni muziki wa kidunia wenye maneno ya Kikristo. Kwa kadiri roho wa dunia hii inavyozidi kujipenyeza Kanisani, si ajabu kuuona muziki wake pia ukiingia Kanisani. Tunapotazama muziki na uimbaji wa Kikristo ulioko sasa hivi, tunapata kuona ni kwa kiasi gani roho ya ulimwengu ilivyolivamia Kanisa. Kwa kadiri uimbaji Kanisani unavyozidi kuchukua sura ya kidunia tunaona jinsi hili linavyoleta kuchanganyikiwa na kumenyana, hasa kwa vijana. Swali ninalotaka kuuliza ni: Je, kuabudu halisi kuna uhusiano gani na muziki wa kidunia? Ninashindwa kuelewa ni kwa nini tutake na hata tujaribu kuyachanganya, haya mawili kumsifu Bwana kwa mdundo wa kidunia kwa kweli, haiwezekani! Tunapokuwa tumezaliwa mara ya pili, tunapaswa tutamani kuabudu kwa mioyo yetu, katika Roho na Kweli. Jambo lolote nje ya hilo ni kuuburudisha mwili. Kwa mara nyingine tena, ninaamini ya kwamba katika kuliangalia Neno la Mungu tutapata ufahamu na ufunuo mpya juu ya moyo wa Mungu katika suala la sifa na kuabudu. Hebu tuwe makini tusikaribishe kila kitu kinachobeba nembo Kristo ya kwamba kinampatia Mungu utukufu. Hakuna maelekezo ya wazi katika Biblia kuhusu namna tunavyopaswa kumuabudu Mungu. Katika Agano la Kale kuna maagizo 32

33 Sura ya IV - Mungu na Muziki yanayohusiana na muziki, kuabudu, na vyombo vya muziki, pamoja na mifano ya watu wa Mungu wakimsifu Mungu kwa shangwe na kucheza; lakini katika Kanisa la Agano Jipya hakuna maelekezo juu ya aina ya maneno, mapigo, au midundo tunayoweza kutumia; au hata namna ya kucheza. Kuna sababu nzuri juu ya hili... kumbuka kuwa sisi ni watu wa Agano Jipya! Kwamba ni weusi au weupe, tajiri au maskini, wasomi au wasio wasomi, sote tuna vitu viwili vinavyofanana: mioyo yetu na Roho Mtakatifu aliyeko ndani yetu. Yeye ni mwalimu wetu, anatuongoza na kutushuhudia mioyoni mwetu juu ya nini kinachotokana na Mungu Baba na nini kisichokuwa cha Mungu. Roho Mtakatifu Ni Mwangalizi Wetu Katika Yohana 16:13-14, tunasoma, Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza mimi; kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari. Hakuna kuchanganya hapa: Ni wazi kwamba Roho Mtakatifu ndiye anayetuelekeza, kutufundisha na kutuongoza katika namna Yesu anavyonena na namna anavyotenda. Sote tutakubaliana kuwa kulikuwa na harufu nzuri ya manukato katika yote Yesu aliyosema na kufanya. Vivyo hivyo, harufu ya manukato ya kumjua Kristo inapaswa iambatane na yote tunayosema na kufanya. Cho chote kinachotokana 33

34 na dunia kina roho nyingine; lakini kwa sababu Mungu ametupa sisi (Wakristo tuliozaliwa mara ya pili) Roho Mtakatifu kuishi ndani ya mioyo yetu, tunaweza kupambanua roho ya ulimwengu huu ulioko chini ya milki ya Shetani. Mambo Ya Ajabu Yanafanyika Ninaamini watu wanaelewa ya kuwa hata katika Ukristo kuna mambo ya misisimko na ya kimwili yanayoendelea. Kwa bahati mbaya si kila kitu chenye nembo ya Ukristo ni kizuri kwa moyo wako au roho yako. Kama ilivyo kwamba kuna aina ya uimbaji na muziki ambavyo tunashuhudiwa mioyoni mwetu ya kuwa vinatokana na Bwana, vivyo hivyo kuna aina ya muziki, uimbaji na kucheza ambavyo vinatoa harufu kali ya kidunia na ya mwili. Tuwe makini tusibebe Neno la Mungu katika hali ya maandiko tu. Neno linaposema Msifuni Bwana kwa vinanda au Msifuni kwa kucheza na shangwe, haina maana kwamba tunaweza kuleta roho ya dunia Kanisani, kwa kucheza kwa namna yoyote tunayojisikia, au kwa kutumia vyombo kucheza midundo au mitindo ambayo huwezi kutofautisha na ile inayochezwa katika kumbi za muziki. Kwa kuangalia mifano michache tu ya kucheza na kushangilia katika Biblia, ninaamini tunaweza kuona tofauti kati ya muziki na kuabudu kunakompendeza Mungu kwa kuashiria kile kilichomo ndani ya 34

35 Sura ya IV - Mungu na Muziki mioyo yetu, na muziki unaotumbuiza tu na kulisha miili yetu, ambao mwisho wake ni kutupeleka katika kutenda dhambi. Katika Kitabu cha 2 Samweli 6:12-15, kuhusiana na wakati ambapo Daudi aliporejesha sanduku la agano, lililowakilisha uwepo wa Mungu katika Yerusalemu, mistari ya inaeleza, Daudi akacheza mbele za BWANA kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani. Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la BWANA kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta. Daudi pamoja na watu wa Israeli walikuwa wanasherehekea ushindi mkubwa. Kicho chake kwa Mungu, unyenyekevu wake, pamoja na furaha ya kweli vilizidi sana ndani yake kiasi cha kumfanya acheze, licha ya kuwa tendo lile lilionekana kama la kipuuzi mbele ya mke wake. Watu walifurahia kile ambacho Mungu alikuwa amefanya, walijua hii haikuwa kazi ya mwanadamu. Daudi alipomuua Goliathi, watu wale wale waliokuwa wakitetemeka kwa hofu ghafla walijawa ujasiri wakatoka kwenda kuwashambulia Wafilisti. Baada ya kuwa wametoka kwenye vita kama hiyo, tunasoma katika 1 Samweli 18:6-7 kwamba, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki Mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda. Nao wanawake wakaitikiana wakicheza. Katika Agano Jipya (Matendo ya Mitume 3) Petro na Yohana walienda hekaluni siku moja, na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa akaponywa. Mtu huyu alishangilia kwa furaha kuu na kucheza ndani ya hekalu akimsifu Mungu kwa muujiza wake. Hakuweza kujizuia katika furaha yake. 35

36 Shangwe Itokayo Moyoni Katika mifano yote mitatu, tunaona mlipuko wa shukrani na shangwe, vilivyotokana na moyo wa shukrani uliosababisha kuimba, kucheza na muziki. Ni suala la Mungu, wala si muziki. Tunaponyenyekezwa na kile ambacho Mungu ametufanyia, tuko huru kufurahia kwa kadiri mioyo yetu itakavyotuongoza. Hakuna tatizo juu ya kuimba na kucheza katika mazingira kama hayo. Lakini viongozi wa sifa wanapoamua Jumapili asubuhi kwamba sasa ni wakati wa kuanza kumsifu Bwana kwa kucheza, au kuabudu kwa kushawishi hisia za watu, kwa uimbaji ambao si kingine bali ni maneno ya Kikristo yaliyoambatana na midundo ya kidunia na yanayotupelekea katika kuigiza, ni lazima tuanze kujiuliza maswali. Na ni vivyo hivyo kwa Matamasha ya Injili. Je, ni nini kinachotokea kwa hawa vijana wa kike na wa kiume ambao hisia zao na miili yao inakuwa imeamshwa kwa hali ya juu na waimbaji walioko jukwaani? Yesu anapewaje heshima na utukufu katika mazingira haya? Wengine wanaweza kusema hiyo ndiyo namna vijana wa kisasa wanavyoabudu na ni njia ya kuwavuta marafiki zao kuja kusikiliza habari za Bwana Yesu. Lakini mimi naweza kuuliza je! ni wangapi katika hawa marafiki wanaofikia kwenye kuzaliwa mara ya pili kwenye haya matamasha? Na, cha muhimu zaidi, je! ni idadi gani ya hawa Wakristo vijana wanaojikuta sasa wakiwa katika barabara ya kurudi nyuma kiroho ikiwa ni matokeo ya kuwasha tamaa 36

37 Sura ya IV - Mungu na Muziki za miili yao kupitia haya matamasha? Mimi binafsi ninapoyasikiliza au kuyatazama matamasha kama haya, Roho Mtakatifu hushuhudia ndani yangu kuwa kuna kitu hakiko sawa. Na sote tunajua ni nani na ni nini kilichoko nyuma ya kila kitu ambacho hakitokani na Roho! Hatuwezi kujificha nyuma ya muziki wa injili unaofurahisha hisia zetu na kuamsha miili yetu. Mwili hauwezi kutoa uzima wa rohoni, kwa hiyo, mara tu mwili unaposisimkia aina fulani ya muziki tuko hatarini. Sisi kama watu wa rohoni ni lazima tuweze kupambanua kati ya muziki utokanao na Mungu - ibada ya moyoni inayojenga - na muziki wa kidunia unaoamsha tu miili na hisia zetu. Muziki Una Vyanzo Viwili Kama tunavyojua, muziki unatokana na mmojawapo ya vyanzo viwili tu. Chanzo cha kwanza ni katika moyo wa Mungu - ambapo wanaume na wanawake, mara nyingi kutokana na kazi ya Mungu waliyoishuhudia maishani mwao, huongozwa na Roho Mtakatifu kutunga sauti au kuandika wimbo. Nyingi za tenzi kuu za Kikristo tulizonazo leo hii zinalishuhudia hili. Mungu ndiye anayeumba huu muziki moyoni mwa mwanadamu ili amwabudu na kumsifu Yeye, kumpa utukufu wote, heshima na uweza. Upako wa Mungu unapokuwepo, mioyo yetu inayeyuka na tunamezwa katika uwepo wake. Chanzo cha pili cha muziki ni roho inayoutawala ulimwengu - ambapo midundo, vionjo na miondoko ni ya kimwili na ya kidunia. 37

38 Muziki ni eneo lingine la hatari sana kwa Kanisa tunapouweka kando msingi, yaani, Injili ya Msalaba, ambayo mara zote inatupa changamoto na kutuleta kwenye utu uzima. Tukikaa kwenye huo msingi, kwa kadiri tunavyozidi kukua na kufanana zaidi na Kristo, tutafahamu pasipo na shaka yo yote ni lipi tufanye, wapi pa kwenda, na kipi cha kusikiliza. Na tutajikuta hatuvutiwi tena na muziki ambao hauifaidi roho kwa namna yoyote. Ninataraji ya kuwa maneno haya machache yameleta mwanga na ufafanuzi zaidi kuhusiana na somo hili; ya kwamba kwa namna fulani Mungu ameyafungua macho yako na umetiwa moyo 38

39 Sura ya V Vita ya Rohoni 39

40 Fundisho lingine ambalo limejipenyeza Kanisani ni lile la vita vya kiroho. Wakristo kila mahali wanatilia mkazo katika kutoa pepo na kudhibiti roho chafu kila mahali wanakokwenda. Ikiwa tunataka kuishi sawasawa na fundisho la uzima la Kristo, tunapaswa tuyachunguze Maandiko tuone ni nini kilichomo moyoni mwa Mungu, na katika mioyo ya Mitume walioandika Nyaraka. Leo hii katika mengi ya makanisa, kuna lugha nyingi na shughuli nyingi linapokuja suala la vita ya rohoni, na kifungu cha Biblia kinachotumika katika hili suala ni Waefeso 6. Hata hivyo, ninapokitazama hiki kifungu, sioni jambo lolote linazungumzia kuanzisha mapambano dhidi ya roho wachafu. Ninachoona ni wito halisi wa Mungu juu ya maisha ya muumini. Mtume Paulo anatuhimiza tujitie nguvu katika Bwana, ili tuweze kusimama siku ya uovu. Mahali pengine, Mtume Yakobo anatuagiza ya kwamba adui ashambuliapo: Mpingeni Shetani naye atawakimbia. Sehemu kubwa ya kile Kanisa linachokiita vita vya kiroho si kingine zaidi ya kupigana na mapepo. Wakristo wanaona hiyo kuwa ndiyo njia ya kupata ushindi maishani mwao. Lakini, Biblia inasema waziwazi ya kuwa ikiwa tuko ndani ya Kristo, Shetani hawezi kutugusa. Ikiwa maisha yetu yako sawa mbele za Mungu, na mioyo yetu ni safi, ni kwa nini tuyaogope mapepo? Tunapaswa tu kuyapinga. Tumeitwa tuishi maisha yenye ushindi, na tutaupata huo ushindi na kupinga mashambulizi ya Shetani tutakapoyafuata maagizo ya Yesu katika Mathayo 16:24: Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. 40

41 Sura ya V - Vita ya Rohoni Tunapoyaangalia Maandiko katika mtazamo sahihi, na kupata ufahamu sahihi wa kile kilichofanyika Msalabani, tutaanza kuona nafasi yetu na msimamo wetu katika Kristo na katika Neno lake. Ninaamini wale wanaojishughulisha na vita vya kiroho wanapaswa wajiulize maswali matatu Vita vya kiroho ni nini hasa? Hili limetajwa wapi kwenye Agano Jipya? Na, Je, dhabihu ya Yesu Msalabani haikutosha? Katika Waefeso 6, ninaamini Mtume Paulo anazungumzia maisha ya ushindi pamoja na Bwana, maisha yenye ushindi katika haki na maisha matakatifu yanayompendeza Mungu. Kwa namna fulani, hii mistari imetafsiriwa kwa namna isiyo sahihi kuleta maana ya kwamba vita ya rohoni ni sehemu ya wito wetu. Leo hii, Kanisani kumeingia uelewa fulani ya kwamba, ikiwa tunataka ushindi, tunahitajika muda wote kuwa vitani tukipigana na mapepo, roho chafu, na kila nguvu na mamlaka; kufunga na kufungua roho kila tupatapo nafasi kwa sababu wametuzunguka kila mahali. Hebu tuangalie mistari ya 10-11: Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, n.k... Kusudi la hili andiko sio kutufundisha jinsi ya kupigana vita ya rohoni. Wito uliopo hapa ni kwamba tuimarike, kwa sababu adui atashambulia! Paulo anasema, Muimarike katika Kristo kwa sababu siku ya uovu imewadia. Mtume anaelewa fika ya kuwa vita au mapambano yo yote maishani mwetu hakika ni ya rohoni, na 41

42 wala si kitu cha kimwili au cha asili. Anatuonya mapema ya kwamba tunapaswa kuwa hodari katika Bwana. Kwa maana nyingine, ikiwa tu imara rohoni hatutashindwa na hila za adui. Ufunguo wa hili ni shauku yetu ya kutaka kukua, na utayari wa kuyasalimisha maisha yetu kikamilifu kwa Kristo. Hapo Bwana atatupa neema ya kusimama, hata kama tu wachanga kiroho, tunapozidi kumpinga Shetani. Mungu hatamruhusu adui avuke mpaka kwani yeye ndiye mlinzi wetu; yeye ni ngao na mwokozi wetu. Shauku kuu ya Paulo ni kwamba tumtumikie Bwana katika hali zote na ya kwamba adui ashambuliapo, tuwe hodari katika imani ili tuweze kusimama imara na kuupata ushindi. Kumtii Mungu Mtume Yakobo anasema katika waraka wake (4:7-8): Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi... Roho iliyoko nyuma ya mistari hii ni sawa na ile iliyo kwenye Waefeso 6; mwito ule ule, maisha yale yale, mamlaka ile ile! Anaposema tuyatiishe maisha yetu kwa Mungu, anamaanisha kujikana nafsi zetu, kuuchukua msalaba wetu, na hatimaye, kumpinga Shetani. 42

43 Sura ya V - Vita ya Rohoni Tutawezaje kubaki mwilini halafu tuende vitani dhidi ya mapepo, na falme, na kudai na kufundisha ya kuwa tutapata ushindi dhidi yao? Huku ni kuyatumia Maandiko kama mbinu, na inakwepa ukweli ya kwamba Ukristo ni maisha tunayoishi katika roho. Silaha Zote Za Mungu Ni vigumu kumshinda Shetani ikiwa hautembei kwenye barabara ya Msalaba na kumruhusu Mungu akutakase na ashughulike na mwili wako. Unaweza ukanukuu kila Andiko, ukafunga kila pepo, ukakiri kila msitari, ukachukua mamlaka dhidi ya kila jambo, na kufunga na kufungua kwa kadiri upendavyo. Ikiwa maisha yako ya rohoni yamevurugika, na hayako juu ya msingi wa Kristo aliyesulubiwa, adui hatakimbia utakapojaribu kumpinga; badala yake, atakuingiza dhambini na kukushinda. Jumbe nyingi zimehubiriwa, na vitabu vimeandikwa, juu ya kuvaa silaha zote za Mungu. Hakika hii haiwezekani iwe ni kanuni ya kimwili; wala haihusikani na kuyanukuu Maandiko, kufunga mapepo, n.k. Si suala la maneno hata kidogo. Silaha yetu ya rohoni inapatikana katika hali za mioyo yetu, maisha yetu matakatifu, na roho wa maombi. Mamlaka yetu inapatikana katika utakatifu wa maisha yetu ya rohoni. Ushindi unapatikana kwenye barabara ya Msalaba! 43

44 Kwa hivyo, je! kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake inamaanisha nini hasa kwa maisha yetu ya siku kwa siku? Tukiunganisha yale wanayoyasema Paulo na Yakobo, ni kwamba ni wakati tunapoyaweka maisha yetu katika mkono hodari wa Bwana. Ni wakati tunapoifungua mioyo yetu kwa ajili ya kuupokea ufunuo wa injili na kumruhusu Mungu kutenda kazi ndani yetu, inayotupeleka kwenye maisha ya imani, haki, maombi, n.k. kwa maana nyingine, tunazivaa silaha zote za Mungu. Kwa jinsi hiyo tunaupata ushindi bila kumenyana na mapepo mchana kutwa. Na, Shetani anapokuja, tunahitajika tu kumpinga bila kufanya jambo lingine zaidi. Huo ndio wito, ndugu na dada zangu. Si kuingia kwenye mapambano ya kiroho dhidi ya mapepo Maisha yetu yanapokuwa juu ya msingi sahihi, tunakuwa na mamlaka ya Mungu katika kumpinga Shetani. Kila anaposhambulia na sisi kumpinga, Shetani hana budi kukimbia. Sote tunakubali ya kuwa mapepo na roho chafu wapo, ila Yesu Kristo amewashinda wote (Wakolosai 2:15). Ndio maana, maisha yetu yanapokuwa yametiishwa kwa Mungu, hatutaogopa mapepo, wala kuyatafuta kila mahali. Mamlaka Ya Mungu Hebu sasa tuangalie Mathayo 16: Yesu anasema, Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga 44

45 Sura ya V - Vita ya Rohoni kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. Bwana wetu alimpa Petro mamlaka kuliongoza Kanisa lake. Anamwambia, Lo lote utakaloamua na kutamka duniani kulingana na mpango wangu na mapenzi yangu, kwa manufaa ya Ufalme, nitakutetea nikiwa mbinguni na nitalifanikisha. Mfano wa hii mamlaka ikitenda kazi unaonekana katika Matendo 5. Akiwa mtu wa imani na maombi, aliyeishi maisha matakatifu na ya haki, Petro alivaa silaha za Mungu, na akaongozwa na Roho Mtakatifu kunena sawasawa na mapenzi ya Mungu. Akafahamu kile Anania na Safira walichokuwa wamekifanya, na akanena kwa mamlaka ya Mungu. Alichofunga duniani kikafungwa na mbinguni. Ninamwona Petro akitekeleza jukumu lake la uongozi, pamoja na mamlaka aliyopewa na Bwana. Kumpinga Shetani Mara nyingine tunahitajika kumpinga Shetani, na kumzuia na kumsimamisha katika kazi zake. Lakini hii haiwezi kuwa mbinu tutakayotumia katika maisha yetu ya siku kwa siku. Paulo na Sila walipowekwa gerezani, hawakuanzisha kipindi cha vita ya rohoni; Biblia inasema walianza kumtukuza Mungu. 45

46 Hawakuhitaji kufunga mapepo au roho yo yote ili wafunguliwe. Mioyo yao ilikuwa sawa, maisha yao yalikuwa kwenye utaratibu wa roho na walimwabudu Mungu, huku wakifahamu ya kuwa ukombozi wao ulikuwa karibu. Muda si mrefu, Mungu akalitikisa gereza na kuwaokoa. Paulo alipofika Athene, Biblia inasema alichukizwa na sanamu na miungu waliyoiabudu. Je, Mtume alianza kufunga mapepo? Hapana! Alinena waziwazi, akiwaambia ya kuwa waliabudu kila aina ya miungu, ila yeye angewaambia habari za Yule waliyepaswa kumwabudu. Akanena habari za Mungu wake, na akawahubiria habari za Yesu Kristo. Tunaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume, tunaona wanafunzi walitumia muda wao wakiihubiri Injili. Walipokutana na mazingira ya kuhitaji kumpinga adui, walifanya hivyo na kuendelea na kazi ya huduma. Hebu tusitekwe akili na kutumia muda mwingi tukishughulika na mapepo, badala ya kuiishi na kuishiriki Injili, na kumtumikia Kristo kwa mioyo yetu yote. 46

47 Sura ya VI Mahusiano Kabla ya Ndoa 47

48 Kama kuna eneo Kanisani leo ambapo kuna mkanganyiko mwingi, na ambapo kuna ushahidi ya kwamba mfumo wa ulimwengu umejipenyeza tena na kuathiri namna Wakristo wanavyofikiri na kuenenda, ni katika mahusiano kabla ya ndoa. Ingawa hili somo linaweza kuonekana kama linawahusu tu vijana wanaotaraji kufunga ndoa, ukweli ni kwamba ni jambo linalohusika na Wakristo wote. Katika hili suala, Kanisa linaonekana kuamua kuchukua mitazamo miwili inayokinzana kabisa. Leo hii tunaona ama sheria au uhuru usiokuwa na mipaka. Katika baadhi ya makanisa kuna sheria kuhusu kile watu wanachoruhusiwa kufanya au kutokufanya, ilhali katika mengine, hilo suala halizungumziwi kabisa. Hakuna mmojawapo ya hii misimamo ulio sahihi! Ninaamini kwa dhati ya kwamba Kanisa limeutelekeza wajibu wake kwa kutokuchukua msimamo wa wazi wa Kibiblia kuhusu namna Wakristo, na hasa vijana, wanavyopaswa kuishi maisha halisi ya Ukristo, iwe ni kabla ya au baada ya kufunga ndoa. Katika kukaa kimya na kuruhusu viwango na fikra za kidunia kuingia Kanisani, tumeacha kuisimamia Kweli ya Injili, na tumejichanganya. Matokeo yake ni kwamba Wakristo wanajiingiza kwenye mahusiano yasiyokuwa ya rohoni na ambayo hayawasaidii kukua na kumtumikia Bwana katika njia sahihi na mara nyingi yakiwapelekea katika kutenda dhambi na kuwaondoa mbali na mpango wa Mungu kwa maisha yao. 48

49 Sura ya VI - Mahusiano Kabla ya Ndoa Kwa ujuzi nilionao ninafahamu ya kwamba Injili inapoyakamata maisha ya vijana, hawamenyani, au kuhisi kusukumwa au kuchanganyikiwa juu ya kile kinachoruhusiwa katika mahusiano yao, au ni wapi wanapaswa kuchora msitari. Kinyume chake, hawahitaji sheria za kuwaambia ni lipi wafanye na lipi wasifanye. Wanafahamu waziwazi mpango wa Mungu ni upi juu ya maisha yao na wanatamani kutenda mapenzi ya Mungu, kubaki wasafi, na kuenenda katika njia inayompendeza Mungu. Tunapoliangalia Neno la Mungu katika mtazamo wake, ninashawishiwa kufikiri ya kwamba dhana zetu kuhusu kuchumbiana, kuwa na marafiki wa kike na marafiki wa kiume, na mahusiano kwa ujumla zitabadilika! Ulimwenguni, mahusiano ya karibu ya kimwili kabla na nje ya ndoa yanakubalika, na hata kushabikiwa. Vipindi vya uchumba vinahesabika kama nyakati za wahusika hao wawili kuona kama wanafaana. Hili mara nyingi linawapelekea katika kuwa na mahusiano ya kimwili kabla ya ndoa. Inasikitisha kwamba katika makanisa mengi vijana wanauiga mtindo huu huu, na wale walio katika nafasi za mamlaka viongozi wa kanisa, wazazi, n.k., hawashughuliki na hili suala kwa umakini unaohitajika. Vijana wanaachiwa kujiamulia wenyewe mipaka katika hili suala nyeti, badala ya kupewa miongozo ya Kibiblia iliyo wazi. Hebu tuwe wazi tokea mwanzo ya kwamba Mungu hachanganyikani; Neno lake halijaficha jambo. Ndani mwake, tunaona maono na 49

50 mpango wake ulio dhahiri, kwa watu wake na kwa Kanisa lake. Ni wazi kwamba hataki tujichanganye na ulimwengu na njia zake. Na wala Mungu hataki sheria na kuhukumiana Kanisani mwake, ambavyo havina nguvu yoyote ya kumbadilisha mtu. Anachotaka ni Wakristo wote wahakikishiwe na Roho Mtakatifu kuhusu dhambi kupitia Injili ya Yesu Kristo ambayo inaweka mpaka ulio wazi na kutuonyesha tunapaswa tusimame juu ya msingi upi. Hii ndiyo maana ninaamini tunapaswa kurejea kwenye msingi Neno la Mungu ili tuone Mungu anasemaje juu ya hili suala. Miili Yetu Ni Viungo Vya Kristo Hebu tuangalie Mungu anavyoiona ndoa na mahusiano nje ya ndoa, na tutafahamu ya kwamba uhusiano wowote wa kimwili nje ya ndoa, uwe wa aina yo yote ile, unahesabika kuwa ni dhambi machoni pa Mungu. Si suala la Tuweke wapi mipaka? kwa sababu tukijaribu kuweka mipaka ya aina yoyote, tutaivuka tu. Ni kama lile tangazo la breki za magari lisemalo, Usianzishe jambo ambalo hutaweza kulizuilia! 1 Wakorintho 6:15 inasema: Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Kwa hivyo, si roho zetu tu zilizounganika na Kristo; nafsi yetu yote ni moja naye. Mistari ya inasema, Au hamjui 50

51 Sura ya VI - Mahusiano Kabla ya Ndoa ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. Paulo hapa anasema waziwazi ya kwamba ni lile tendo la ndoa linalowaunga watu wawili kuwa mwili mmoja, na hili linapaswa kuchukuliwa kwa uzito. Katu hatupaswi kusahau ya kuwa roho zetu, nafsi zetu na miili yetu imeungwa pamoja na Kristo. Siku hizi Wakristo wengi wanafanya wanavyopenda na miili yao, pasipo kutambua madhara ya rohoni yanayotokana na matendo yao. Kwenye kifungu hiki Paulo anaweka utofauti kati ya dhambi ya mwili na dhambi nyingine; katika zinaa unatenda dhambi dhidi ya mwili wako kwa sababu unafanyika kuwa mmoja na yule mnayeunganika naye kimwili. Uzinzi ni uhusiano wowote wa kimwili nje ya ndoa. Uongo, wizi, hasira, n.k., ni tofauti; haya ni matunda ya tamaa zetu za kimwili. Ikiwa Mungu aliamua kuweka utofauti kati ya dhambi ya mwili na dhambi nyingine, tunapaswa kuwa makini sana, na kuufahamu moyo wake katika hili suala. Msitari wa 18 unasema, Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Hatupaswi kusahau ya kuwa miili yetu pamoja na roho zetu vimeungwa na Kristo, na tunapotenda zinaa ni jambo zito sana machoni pa Mungu. Mistari ya inatukumbusha ya kuwa mwili wetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na tunahimizwa, mtukuzeni Mungu katika miili yenu. 51

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA BILL SUPPLEMENT

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA BILL SUPPLEMENT ISSN 0856-035X THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA BILL SUPPLEMENT No. 6 20 th February, 2015 to the Gazette of the United Republic of Tanzania No.8 Vol.96 dated 20 th February, 2015 Printed by the Government

More information

TUNGO ZA KUJIBIZANA: "KUAMBIZANA NI SIFA YA KUPENDANA"t

TUNGO ZA KUJIBIZANA: KUAMBIZANA NI SIFA YA KUPENDANAt AAP 47 (1996) 1-10 TUNGO ZA KUJIBIZANA: "KUAMBIZANA NI SIFA YA KUPENDANA"t RIDDER SAMSOM Different labels have been used for marking the reciprocity in Swahili dialogue poetry, varying between the more

More information

MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO

MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO NEW LIFE IN CHRIST SERIES 1 MAISHA MAPYA NDANI YA KRISTO FISHERS OF MEN MINISTRIES CHURCH NAME 2 Fishers of Men Ministries uses a Christ centered approach to transform one life at a time by feeding their

More information

Contents Page. 3. Financial Highlights 4-8. Chairman s Statement 9-12. CEO s Statement

Contents Page. 3. Financial Highlights 4-8. Chairman s Statement 9-12. CEO s Statement Contents Page 01 HIGHLIGHTS 3. Financial Highlights 4-8. Chairman s Statement 9-12. CEO s Statement 02 BUSINESS REVIEW 14. The Value We Have Created 15-16. What We Do 17. How We Are Managed 20-21. Who

More information

Annual Report and Financial Statements

Annual Report and Financial Statements 2013 Annual Report and Financial Statements 2 2013 Annual Report and Financial Statements Our Vision To be a dynamic company committed to exceeding customer expectation and increasing our market share

More information

Ni Wakati Wa Kuamka! Ellis P. Forsman. Ni Wakati Wa Kuamka (It's Time To Wake Up) 1

Ni Wakati Wa Kuamka! Ellis P. Forsman. Ni Wakati Wa Kuamka (It's Time To Wake Up) 1 Ni Wakati Wa Kuamka! na Ellis P. Forsman Ni Wakati Wa Kuamka (It's Time To Wake Up) 1 Ni Wakati Wa Kuamka! na Ellis P. Forsman Oktoba 12, 2011 Ni Wakati Wa Kuamka (It's Time To Wake Up) 2 Ni Wakati Wa

More information

THE OIL AND GAS REVENUES MANAGEMENT ACT, 2015 ARRANGEMENT OF SECTIONS PART I PRELIMINARY PROVISIONS PART II ADMINISTRATIVE PROVISIONS

THE OIL AND GAS REVENUES MANAGEMENT ACT, 2015 ARRANGEMENT OF SECTIONS PART I PRELIMINARY PROVISIONS PART II ADMINISTRATIVE PROVISIONS ISSN 0856-035X THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA BILL SUPPLEMENT No. 10 29 th May, 2015 to the Gazette of the United Republic of Tanzania No. 22 Vol. 96 dated 29 th May, 2015 Printed by the Government Printer,

More information

Linking Adult Education with Formal Schooling in Tanzania: Mission Unfulfilled

Linking Adult Education with Formal Schooling in Tanzania: Mission Unfulfilled Linking Adult Education with Formal Schooling in Tanzania: Mission Unfulfilled Mohamed Salum Msoroka Faculty of Education School of Educational Leadership & Policy The University of Waikato Contact Address:

More information

TANZANIA COFFEE BOARD VACANCIES ANNOUNCEMENT

TANZANIA COFFEE BOARD VACANCIES ANNOUNCEMENT TANZANIA COFFEE BOARD VACANCIES ANNOUNCEMENT Tanzania Coffee Board is a government body established by the Tanzania Coffee Industry Act No. 23 of 2001. Its main function is to regulate the coffee industry

More information

Contents. CORE VALUES Integrity Professionalism Team Spirit Safety Culture. Company Information 2 Message from the Chairman 4

Contents. CORE VALUES Integrity Professionalism Team Spirit Safety Culture. Company Information 2 Message from the Chairman 4 A N N U A L R E P O RT & F I N A N C I A L S TAT E M E N T S Financial year ended 30 June 2010 Contents Company Information 2 Message from the Chairman 4 VISION To be the market leader in the provision

More information

MARX'S SHORTS AND ANCESTORS' CAVES: TRACING CRITICAL MOTIFS IN KEZILAHABI'S PLAY AND POEMS*

MARX'S SHORTS AND ANCESTORS' CAVES: TRACING CRITICAL MOTIFS IN KEZILAHABI'S PLAY AND POEMS* AAP 47 (1996). 139-148 MARX'S SHORTS AND ANCESTORS' CAVES: TRACING CRITICAL MOTIFS IN KEZILAHABI'S PLAY AND POEMS* ELENA BER TONCINI-ZUBKOV A La seule piece theiitrale de Kezilahabi, "Les shorts de Marx",

More information

TANZANIA AND HIV/AIDS TANZANIA NA UKIMWI

TANZANIA AND HIV/AIDS TANZANIA NA UKIMWI TANZANIA AND HIV/AIDS TANZANIA NA UKIMWI This booklet, which summarizes key findings on HIV/AIDS, is based on surveys and other studies conducted over the past decade in Tanzania. Major data sources include

More information

Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake?

Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake? JE! MUNGU HABADILISHA NIA YAKE KUHUSU NENO LAKE? 1 Je! Mungu Habadilisha Nia Yake Kuhusu Neno Lake? ` Na tuinamishe vichwa vyetu. Bwana Yesu mpenzi, tumekusanyika tena katika Jina Lako, tukiwa na matumaini

More information

Ndugu na dada zangu. Mbio za Maisha

Ndugu na dada zangu. Mbio za Maisha UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2012 Na Rais Thomas S. Monson Mbio za Maisha Sisi tulitoka wapi? Kwa nini tuko hapa? Tutaenda wapi baada ya maisha haya? Haya maswali ya kawaida hayafai kubaki bila kujibiwa.

More information

Toleo No. 51 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Tarehe - 23-29 Januari, 2015

Toleo No. 51 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Tarehe - 23-29 Januari, 2015 HABARI Habari ZA za NISHATI nishati &MADINI &madini Bulletin Toleo No. 51 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM Tarehe - 23-29 Januari, 2015 Toleo No. 78 Limesambazwa kwa Taasisi na Idara zote MEM

More information

EXISTENTIALISM AND FEMINISM IN KEZILAHABI S NOVEL KICHWAMAJI

EXISTENTIALISM AND FEMINISM IN KEZILAHABI S NOVEL KICHWAMAJI SWAHILI FORUM 15 (2008): 51-61 EXISTENTIALISM AND FEMINISM IN KEZILAHABI S NOVEL KICHWAMAJI TIINA SAKKOS Makala hii inachambua riwaya ya pili ya mwandishi maarufu wa Kiswahili, Euphrase Kezilahabi (*1944)

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SABOTI CONSTITUENCY, HELD AT KITALE TOWN MUSEUM HALL

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SABOTI CONSTITUENCY, HELD AT KITALE TOWN MUSEUM HALL CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SABOTI CONSTITUENCY, HELD AT KITALE TOWN MUSEUM HALL ON 2 1 ST JULY 2002 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS SABOTI

More information

Lesson 56: Business: [biashara: ununuzi, upigaji bei na uuzaji] Business: Shopping, Buying and Selling. A). Business Vocabulary.

Lesson 56: Business: [biashara: ununuzi, upigaji bei na uuzaji] Business: Shopping, Buying and Selling. A). Business Vocabulary. Lesson 56: Business: Shopping, Buying and Selling Business: Shopping, Buying and Selling [biashara: ununuzi, upigaji bei na uuzaji] A). Business Vocabulary akaunti akiba bei ghali rahisi bei ghali bei

More information

Annual Report Report and and Financial Statements

Annual Report Report and and Financial Statements Annual Report Report and and Financial Statements For For the the Year Year ended ended 31 31 March March 2014 2014 Dreams into into reality KQ Annual Report & Financial Statements 2014 1 Performance Highlights

More information

ROMAN CATHOLIC FAITH REPRESENTED IN KEZILAHABI'S MZINGILE SONJA MEZGER AAP 72 (2002) SWAHILI FORUM IX 75-85

ROMAN CATHOLIC FAITH REPRESENTED IN KEZILAHABI'S MZINGILE SONJA MEZGER AAP 72 (2002) SWAHILI FORUM IX 75-85 AAP 72 (2002) SWAHILI FORUM IX 75-85 ROMAN CATHOLIC FAITH REPRESENTED IN KEZILAHABI'S MZINGILE SONJA MEZGER Summary This study elaborates how Kezilahabi depicts elements of Roman Catholic faith in his

More information

DAR ES SALAAM UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION. A Constituent College of the University of Dar Es Salaam STAFF FUNERAL POLICY

DAR ES SALAAM UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION. A Constituent College of the University of Dar Es Salaam STAFF FUNERAL POLICY DAR ES SALAAM UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION A Constituent College of the University of Dar Es Salaam STAFF FUNERAL POLICY JANUARY 2015 TABLE OF CONTENTS 1 BACKGROUND... 1 2 THE ROLE OF THE EMPLOYER...

More information

OPERATIONS MANUAL FOR IMPLEMENTATION AND MANAGEMENT OF A COMMUNITY HEALTH FUND in Tanga Region

OPERATIONS MANUAL FOR IMPLEMENTATION AND MANAGEMENT OF A COMMUNITY HEALTH FUND in Tanga Region 1 OPERATIONS MANUAL FOR IMPLEMENTATION AND MANAGEMENT OF A COMMUNITY HEALTH FUND in Tanga Region A MANUAL FOR PRACTITIONERS Second edition January 2006 Contacts The Regional CHF Competence Center (RCCC),

More information

Creation of a Speech to Text System for Kiswahili

Creation of a Speech to Text System for Kiswahili Creation of a Speech to Text System for Kiswahili Dr. Katherine Getao and Evans Miriti University of Nairobi Abstract The creation of a speech to text system for any language is an onerous task. This is

More information

Centum Investment Company Limited Annual Report & Financial Statements fy 13/14

Centum Investment Company Limited Annual Report & Financial Statements fy 13/14 Centum Investment Company Limited Annual Report & Financial Statements fy 13/14 Africa s Foremost Investment Channel At Centum, we focus on sustainable wealth creation, leveraging on teamwork and the expertise

More information

Lesson 14a: Numbers and Counting

Lesson 14a: Numbers and Counting Lesson 14a: Numbers and Counting Numbers and Counting [nambari na hesabu] A). Numbers B). The order in which the numbers are stated C). How numbers and noun class [ngeli] go together D). Questions with

More information

KUKITANDAWAZISHA KISWAHILI KUPITIA SIMU ZA KIGANJANI: TAFAKARI KUHUSU ISIMUJAMII

KUKITANDAWAZISHA KISWAHILI KUPITIA SIMU ZA KIGANJANI: TAFAKARI KUHUSU ISIMUJAMII SWAHILI FORUM 18 (2011): 198-210 KUKITANDAWAZISHA KISWAHILI KUPITIA SIMU ZA KIGANJANI: TAFAKARI KUHUSU ISIMUJAMII ALDIN MUTEMBEI Utangulizi Mojawapo ya matokeo ya utandawazi ni kuwapo kwa simu za kiganjani

More information

Kitabu hiki kimefanikishwa kwa msaada wa Taasisi ya Bill na Melinda Gates

Kitabu hiki kimefanikishwa kwa msaada wa Taasisi ya Bill na Melinda Gates Kitabu hiki kimefanikishwa kwa msaada wa Taasisi ya Bill na Melinda Gates Programu ya Teknolojia Inayofaa kwenye Afya (PATH) inatoa masuluhisho endelevu, yanayofaa kiutamaduni na ambayo inawezesha jamii

More information

815 SWA. Health undertaking Kuwajibika Kiafya. Tafadhali weka kurasa hii ya maelezo kama kumbukumbu yako

815 SWA. Health undertaking Kuwajibika Kiafya. Tafadhali weka kurasa hii ya maelezo kama kumbukumbu yako Health undertaking Kuwajibika Kiafya Form 815 SWA SWAHILI Muhimu Tafadhali soma maelezo haya kwa uangalifu kabla ya kukamilisha wajibu wako. Mara tu unapokamilisha wajibu wako tunashauri kwa nguvu kuwa

More information

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, HOTUBA YA MWENYEKITI WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA, MHE. JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA, AKIWASILISHA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KATIKA BUNGE MAALUM LA KATIBA, MACHI 2014 UTANGULIZI

More information

Yaliyomo. II. Dodoso la Kilimo... 62

Yaliyomo. II. Dodoso la Kilimo... 62 OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU Mwongozo wa Mdadisi Utafiti wa Kufuatilia Kaya Tanzania (NPS 2010-11) 2010-2011 0 [JAMHURI YA MUUNGA N O W A TANZA N I A] Yaliyomo Comment [SP1]: Be sure to update the table of

More information

Uundaji wa Istilahi za Kiswahili Kileksikografia na Athari zake S.S. SEWANGI University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Uundaji wa Istilahi za Kiswahili Kileksikografia na Athari zake S.S. SEWANGI University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(3): 333 344 (2007) Uundaji wa Istilahi za Kiswahili Kileksikografia na Athari zake S.S. SEWANGI University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT The promotion of terminology

More information

THE ANTI-MONEY LAUNDERING ACT,2006

THE ANTI-MONEY LAUNDERING ACT,2006 THE ANTI-MONEY LAUNDERING ACT,2006 ARRANGEMENT OF SECTIONS Section Title PART I PRELIMINARY PROVISIONS 1. Short title and Commencement 2. Application. 3. Interpretation. PART II THE FINANCIAL INTELLIGENCE

More information

CONTENTS. Financial Section. Sehemu ya Kiswahili. Statutory Information

CONTENTS. Financial Section. Sehemu ya Kiswahili. Statutory Information CONTENTS Financial Highlights 3 Chairman s Statement 4-5 Production 6-8 Brands 10-12 Human Resource 13 Enriching Communities 14-15 Sehemu ya Kiswahili Taarifa ya Mwenyekiti 16-17 Utaoji 18-20 Aina za Bidhaa

More information

Tunza Jamii Yako, Tunza Mazingira Yako kwa Maisha Bora. Jihusishe. Jipangie. Amua

Tunza Jamii Yako, Tunza Mazingira Yako kwa Maisha Bora. Jihusishe. Jipangie. Amua Tunza Jamii Yako, Tunza Mazingira Yako kwa Maisha Bora. Jihusishe. Jipangie. Amua Orodha ya kukagua matayarisho: Soma hadithi yote mapema pamoja na maelezo ya hadithi na maswali ya kukukumbusha. Tayarisha

More information

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI

More information

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF

CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, NAMBALE CONSTITUENCY, HELD AT MATAYOS LWANYA GIRLS SEC. SCHOOL ON 29 TH JULY 2002 2 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS,

More information

CUF. Rais makini, Serikali makini Uchumi Imara, Mabadiliko Sahihi

CUF. Rais makini, Serikali makini Uchumi Imara, Mabadiliko Sahihi CUF Rais makini, Serikali makini Uchumi Imara, Mabadiliko Sahihi The Civic United Front (CUF-Chama Cha Wananchi) Yaliyomo 1. Utangulizi wa Prof Ibrahim Lipumba... 7 2. Misingi mikuu ya uongozi wa nchi...

More information

Mwalimu Nyerere Engages His People: Scripture Translation in Swahili Verse

Mwalimu Nyerere Engages His People: Scripture Translation in Swahili Verse Journal of Translation, Volume 3, Number 1 (2007) 41 Mwalimu Nyerere Engages His People: Scripture Translation in Swahili Verse Phil Noss and Peter Renju 1 Phil Noss was the UBS Translation Services Coordinator

More information

ANNUAL REPORT 2015 THE TASKS OF TBL INTRODUCING

ANNUAL REPORT 2015 THE TASKS OF TBL INTRODUCING THE HOME OF FINE BEERS ANNUAL REPORT 2015 INTRODUCING THE TASKS OF TBL PROUDLY TANZANIAN SINCE 1933 A subsidiary of SABMiller plc To Be a Good Corporate Citizen To Invest in Our Country To Invest in Our

More information

TEGENI MASIKIO: COMPOSING EAST AFRICAN REALITIES THROUGH YOUNG EYES

TEGENI MASIKIO: COMPOSING EAST AFRICAN REALITIES THROUGH YOUNG EYES SWAHILI FORUM 19 (2012): 45-59 TEGENI MASIKIO: COMPOSING EAST AFRICAN REALITIES THROUGH YOUNG EYES AARON LOUIS ROSENBERG At times creative writing has been employed by Tanzanians in order to demonstrate

More information

A SHABA SWAHILI LIFE HISTORY: TEXT AND TRANSLATION

A SHABA SWAHILI LIFE HISTORY: TEXT AND TRANSLATION AAP 42 (1995). 73-103 A SHABA SWAHILI LIFE HISTORY: TEXT AND TRANSLATION JAN BLOMMAERT Intruduction This paper presents an edited version of a handwritten text in Shaba Swahili and French, accompanied

More information

LEARNING HOW TO TEACH

LEARNING HOW TO TEACH Education International Internationale de l Education Internacional de la Educación Bildungsinternationale LEARNING HOW TO TEACH The upgrading of unqualified primary teachers in sub-saharan Africa Lessons

More information

Tuko Pamoja. Adolescent Reproductive Health and Life Skills Curriculum

Tuko Pamoja. Adolescent Reproductive Health and Life Skills Curriculum Tuko Pamoja Adolescent Reproductive Health and Life Skills Curriculum Tuko Pamoja Adolescent Reproductive Health and Life Skills Curriculum Acknowledgements This second edition of the Kenya Adolescent

More information

TAARIFA YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UKIMWI MKOA WA KIGOMA

TAARIFA YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UKIMWI MKOA WA KIGOMA TUME YA KUDHIBITI UKIMWI TANZANIA (TACAIDS) TAARIFA YA UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UKIMWI MKOA WA KIGOMA OKTOBA, 2007 ISBN 978-9987-519-18-7 i ii Yaliyomo Ufafanuzi wa Majedwali Vifupisho Shukrani Muhtasari

More information

Language Choice in Swahili Newspaper Advertising in Tanzania

Language Choice in Swahili Newspaper Advertising in Tanzania US-China Foreign Language, ISSN 1539-8080 June 2013, Vol. 11, No. 6, 447-460 D DAVID PUBLISHING Language Choice in Swahili Newspaper Advertising in Tanzania Josephine Dzahene-Quarshie University of Ghana,

More information

LUGHA YA MITAANI IN TANZANIA THE POETICS AND SOCIOLOGY OF A YOUNG URBAN STYLE OF SPEAKING

LUGHA YA MITAANI IN TANZANIA THE POETICS AND SOCIOLOGY OF A YOUNG URBAN STYLE OF SPEAKING SWAHILI FORUM 13 Edited by: Rose Marie Beck, Lutz Diegner, Clarissa Dittemer, Thomas Geider, Uta Reuster-Jahn SPECIAL ISSUE LUGHA YA MITAANI IN TANZANIA THE POETICS AND SOCIOLOGY OF A YOUNG URBAN STYLE

More information

Sda Church Nyimbo Za Kristo

Sda Church Nyimbo Za Kristo Sda Nyimbo Za Kristo Free PDF ebook Download: Sda Nyimbo Za Kristo Download or Read Online ebook sda church nyimbo za kristo in PDF Format From The Best User Guide Database Apr 27, 2011 - Saturday. EAT

More information

MORE SWAHILI PROVERBS FROM EAST AFRICA METHALI ZAIDI ZA KISWAHILI TOKA AFRIKA MASHARIKI. L. Kalugila. A. Y. Lodhi

MORE SWAHILI PROVERBS FROM EAST AFRICA METHALI ZAIDI ZA KISWAHILI TOKA AFRIKA MASHARIKI. L. Kalugila. A. Y. Lodhi MORE SWAHILI PROVERBS FROM EAST AFRICA METHALI ZAIDI ZA KISWAHILI TOKA AFRIKA MASHARIKI L. Kalugila A. Y. Lodhi Scandinavian Institute of African Studies, Uppsala 1980 MORE SWAHILI PROVERBS FROM EAST AFRICA

More information

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA JAMII MKOA WA DODOMA

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA JAMII MKOA WA DODOMA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA JAMII MKOA WA DODOMA Kimetayarishwa kwa Ushirikiano Kati ya: TUME YA MIPANGO DAR ES SALAAM na OFISI YA MKUU WA MKOA DODOMA YALIYOMO Ukurasa

More information

The Usage of Kiswahili in Blog Discourse and the Effect on Its Development

The Usage of Kiswahili in Blog Discourse and the Effect on Its Development International Journal of Humanities and Social Science Vol. 3 No. 14 [Special Issue - July 2013] The Usage of Kiswahili in Blog Discourse and the Effect on Its Development Juliet Akinyi Jagero Jaramogi

More information

Lesson 24: Adjectives

Lesson 24: Adjectives Lesson 24: Adjectives Adjectives [vivumishi vya sifa] Adjectives are formed by attaching the noun class marker to an adjectival stem. Adjectives have various properties: Word origin (e.g. Bantu, Arabic)

More information

CURRICULUM INNOVATION IN TEACHER EDUCATION

CURRICULUM INNOVATION IN TEACHER EDUCATION CURRICULUM INNOVATION IN TEACHER EDUCATION Curriculum Innovation in Teacher Education Exploring Conceptions among Tanzanian Teacher Educators Wilberforce E. Meena ÅBO 2009 ÅBO AKADEMIS FÖRLAG ÅBO AKADEMI

More information

Celebration of the French «Bastille Day» Remarks by Ambassador Elisabeth Barbier 14th July 2010

Celebration of the French «Bastille Day» Remarks by Ambassador Elisabeth Barbier 14th July 2010 Celebration of the French «Bastille Day» Remarks by Ambassador Elisabeth Barbier 14th July 2010 Honorable Ministers, Dear colleagues, compatriots and friends, Mabibi na Mabwana, First of all, let me, together

More information

KISWAHILI Pam Inoti - pamby22@gmail.com

KISWAHILI Pam Inoti - pamby22@gmail.com KISWAHILI Pam Inoti - pamby22@gmail.com Kiswahili is a national and official language in Kenya, Tanzania and Uganda. It is also spoken in Rwanda, Burundi, Congo (DRC), Somalia, Comoros Islands (including

More information

P.O. Box 4374 DAR ES SALAAM TEL:+255 22 2775915/6 FAX: +255 22 2775915 E-mail:itv@ipp.co.tz www.ippmedia.com

P.O. Box 4374 DAR ES SALAAM TEL:+255 22 2775915/6 FAX: +255 22 2775915 E-mail:itv@ipp.co.tz www.ippmedia.com S/N NAME OF LICENSEE ADDRESS 1. Radio One P.O. Box 4374 TEL:+255 22 2775915/6 FAX: +255 22 2775915 itv@ipp.co.tz www.ippmedia.com AUTHORIZED SERVICE AREA AND LOCATION OF BASE STATION ( Dar es AUTHORIZED

More information

TRAINING ON ENTREPRENEURSHIP AND BUSINESS MANAGEMENT SKILLS FOR SELECTED VILLAGERS IN RUFIJI

TRAINING ON ENTREPRENEURSHIP AND BUSINESS MANAGEMENT SKILLS FOR SELECTED VILLAGERS IN RUFIJI TANZANIA COUNTRY OFFICE TRAINING ON ENTREPRENEURSHIP AND BUSINESS MANAGEMENT SKILLS FOR SELECTED VILLAGERS IN RUFIJI August 2009 University of Dar es Salaam Entrepreneurship Centre (UDEC) P. O. Box 110099,

More information

Teach Yourself Swahili

Teach Yourself Swahili Teach Yourself Swahili Hassan O. Ali & Ali M. Mazrui August 3, 2004 Contents ABOUT THIS COURSE... 1 ABOUT SWAHILI... 1 LESSON 1: ALPHABET... 3 LESSON 2: PRONUNCIATION GUIDE... 3 VOWELS... 3 SYLLABLES...

More information

The mother, her confidants and the prevention of mother-to-child transmission of HIV (PMTCT) services in the Kilimanjaro region, Tanzania

The mother, her confidants and the prevention of mother-to-child transmission of HIV (PMTCT) services in the Kilimanjaro region, Tanzania The mother, her confidants and the prevention of mother-to-child transmission of HIV (PMTCT) services in the Kilimanjaro region, Tanzania Eli Fjeld Falnes Dissertation for the degree philosophiae doctor

More information

DR. HAMISI O. BABUSA (PHD)

DR. HAMISI O. BABUSA (PHD) DR. HAMISI O. BABUSA (PHD) School of Education Department of Educational Communication and Technology Kenyatta University P.O. Box 43844 Nairobi 00100 Kenya Mobile: +254 700 754 080 Email: hobabusa@gmail.com

More information

Promoting Regional Trade to Enhance Food Security

Promoting Regional Trade to Enhance Food Security SLE Publication Series S239 Centre for Advanced Training in Rural Development (SLE) International Institute of Tropical Agriculture (IITA) on behalf of Deutsche Gesellschaft für Technische Zusammenarbeit

More information

MEANING AS USE: A FUNCTIONAL VIEW OF SEMANTICS AND PRAGMATICS

MEANING AS USE: A FUNCTIONAL VIEW OF SEMANTICS AND PRAGMATICS SWAHILI FORUM 11 (2004): 127-139 MEANING AS USE: A FUNCTIONAL VIEW OF SEMANTICS AND PRAGMATICS ALICE MWIHAKI This article addresses the notion of linguistic meaning with reference to Kiswahili. It focuses

More information

Ambassador s Community Grants Fund for HIV/AIDS Relief

Ambassador s Community Grants Fund for HIV/AIDS Relief Ambassador s Community Grants Fund for HIV/AIDS Relief Each year, the United States Ambassador s Community Grants Fund in Tanzania will award HIV/AIDS-focused grants, ranging from $5,000 to $30,000, to

More information

ARMS CONTROL Volume 3 Issue 1 May 2011

ARMS CONTROL Volume 3 Issue 1 May 2011 ARMS CONTROL Volume 3 Issue 1 May 2011 Editorial Welcome to the first Issue of the third volume of Arms Control: Africa, which is published by the Arms Management Programme (AMP) of the Institute for Security

More information

Mother Tongue Theological Education in Africa: A Response to Jim Harries The Prospects for Mother Tongue Theological Education in Western Kenya

Mother Tongue Theological Education in Africa: A Response to Jim Harries The Prospects for Mother Tongue Theological Education in Western Kenya Wildsmith Mother Tongue Theological Education in Africa 17 Mother Tongue Theological Education in Africa: A Response to Jim Harries The Prospects for Mother Tongue Theological Education in Western Kenya

More information

1. TASAF operations steadily approaching set targets

1. TASAF operations steadily approaching set targets 1. TASAF operations steadily approaching set targets The implementation support mission by the World Bank team to TASAF which took place from March 23 rd to April 04 th concluded that TASAF II implementation

More information

TEKNOLOJIA ZA UTAYARISHAJI, USINDIKAJI NA HIFADHI YA MAZAO YA MBEGU ZA MAFUTA BAADA YA KUVUNA. Kitabu Namba 5

TEKNOLOJIA ZA UTAYARISHAJI, USINDIKAJI NA HIFADHI YA MAZAO YA MBEGU ZA MAFUTA BAADA YA KUVUNA. Kitabu Namba 5 1 TEKNOLOJIA ZA UTAYARISHAJI, USINDIKAJI NA HIFADHI YA MAZAO YA MBEGU ZA MAFUTA BAADA YA KUVUNA Kitabu Namba 5 Jamhuri ya Muungano wa Tanzania W izara ya Kilimo na Chakula 1 2 Mfululizo wa vitabu hivi:

More information

Swahili. Information provided by: National African Language Resource Center (NALRC)

Swahili. Information provided by: National African Language Resource Center (NALRC) Swahili Information provided by: National African Language Resource Center (NALRC) A). Why study Swahili? Swahili (or Kiswahili as it is called when one is speaking the language) is the most important

More information

CURRICULUM VITAE PERSONAL DETAILS. Prof. Wanyama Mellitus Nyongesa. Age: 47. Associate Professor of Musicology at Moi University, Eldoret, Kenya

CURRICULUM VITAE PERSONAL DETAILS. Prof. Wanyama Mellitus Nyongesa. Age: 47. Associate Professor of Musicology at Moi University, Eldoret, Kenya CURRICULUM VITAE PERSONAL DETAILS Name: Sex: Prof. Wanyama Mellitus Nyongesa Male Age: 47 Place of Birth: Nationality: Occupation: Bungoma County, Kenya Kenyan Associate Professor of Musicology at Moi

More information

Winners, cheats and witches: East African soccer cartoons Beez, Jigal

Winners, cheats and witches: East African soccer cartoons Beez, Jigal www.ssoar.info Winners, cheats and witches: East African soccer cartoons Beez, Jigal Veröffentlichungsversion / Published Version Zeitschriftenartikel / journal article Empfohlene Zitierung / Suggested

More information

Lesson 43: Commands. D). Commands may take object markers to indicate the recipient of a command

Lesson 43: Commands. D). Commands may take object markers to indicate the recipient of a command Lesson 43: Commands Commands [amri] A). Commands using regular verbs (which generally end in A) when indicating a single recipient will take the normal verb form, but commands indicating multiple recipients

More information

Schneps, Leila; Colmez, Coralie. Math on Trial : How Numbers Get Used and Abused in the Courtroom. New York, NY, USA: Basic Books, 2013. p i.

Schneps, Leila; Colmez, Coralie. Math on Trial : How Numbers Get Used and Abused in the Courtroom. New York, NY, USA: Basic Books, 2013. p i. New York, NY, USA: Basic Books, 2013. p i. http://site.ebrary.com/lib/mcgill/doc?id=10665296&ppg=2 New York, NY, USA: Basic Books, 2013. p ii. http://site.ebrary.com/lib/mcgill/doc?id=10665296&ppg=3 New

More information

The Mosaic Project Theme Song 2001 The Mosaic Project Music by Brett Dennen, Lyrics by Brett Dennen and Lara Mendel

The Mosaic Project Theme Song 2001 The Mosaic Project Music by Brett Dennen, Lyrics by Brett Dennen and Lara Mendel The Mosaic Project Theme Song 2001 The Mosaic Project M is for MUTUAL RESPECT Don't put me down and don't hurt me. O is for OPEN MINDEDNESS See me for who I am and don't judge me. S is for SELF RESPECT

More information

Girls Getting to Secondary School Safely: Combating Gender-based Violence in the Transportation Sector in Tanzania

Girls Getting to Secondary School Safely: Combating Gender-based Violence in the Transportation Sector in Tanzania Girls Getting to Secondary School Safely: Combating Gender-based Violence in the Transportation Sector in Tanzania Laura Mack Center for Gender Equity 2009 In July 2011, FHI 360 acquired the programs,

More information

The United Republic of Tanzania

The United Republic of Tanzania The United Republic of Tanzania Health Services Inspectorate Unit Ministry of Health and Social Welfare Implementation Guideline for 5S-CQI-TQM Approaches in Tanzania Foundation of all Quality Improvement

More information

NEGOTIATING THE NEW TUKI ENGLISH-SW AHILI DICTIONARY A CRITIQUE FROM A PEDAGOGICAL AND SCHOLARLY PERSPECTIVE'

NEGOTIATING THE NEW TUKI ENGLISH-SW AHILI DICTIONARY A CRITIQUE FROM A PEDAGOGICAL AND SCHOLARLY PERSPECTIVE' AAP 51 (1997) 181-218 NEGOTIATING THE NEW TUKI ENGLISH-SW AHILI DICTIONARY A CRITIQUE FROM A PEDAGOGICAL AND SCHOLARLY PERSPECTIVE' THOMAS J.. HINNEBUSCH Intmduction This paper is intended to give a somewhat

More information

Section 2 Assessment

Section 2 Assessment Section 2 Assessment The translation of each phrase is in the following order ARABIC BENGALI CHINESE CZECH FARSI FRENCH GUJARATI HINDI ENGLISH POLISH PORTUGESE PUNJABI SOMALI SWAHILI TURKISH URDU Assessment

More information

INITIAL BEHAVIOR CHANGE COMMUNICATION (BCC) INTERVENTIONS EFFECTIVENESS EVALUATION REPORT

INITIAL BEHAVIOR CHANGE COMMUNICATION (BCC) INTERVENTIONS EFFECTIVENESS EVALUATION REPORT INITIAL BEHAVIOR CHANGE COMMUNICATION (BCC) INTERVENTIONS EFFECTIVENESS EVALUATION REPORT NAFAKA PROJECT November 5, 2013 This publication was produced for review by the United States Agency for International

More information

Towards Full Comprehension of Swahili Natural Language Statements for Database Querying

Towards Full Comprehension of Swahili Natural Language Statements for Database Querying 6 Towards Full Comprehension of Swahili Natural Language Statements for Database Querying Lawrence Muchemi Natural language access to databases is a research area shrouded by many unresolved issues. This

More information

TANZANIA PARALEGAL BASELINE SURVEY

TANZANIA PARALEGAL BASELINE SURVEY TANZANIA PARALEGAL BASELINE SURVEY AUGUST 2010 1.0 INTRODUCTION This is a report on a Paralegal baseline survey conducted in all regions of Tanzania mainland. The baseline survey was commissioned to Tanganyika

More information

L E A P n e w s. Tahariri. Editor s note. Number 15/16 September December 2007 Newsletter of the Language in Education in Africa Project

L E A P n e w s. Tahariri. Editor s note. Number 15/16 September December 2007 Newsletter of the Language in Education in Africa Project L E A P n e w s Number 15/16 September December 2007 Newsletter of the Language in Education in Africa Project Author Niki Daly entertaining a young audience at the Vulindlela Reading Club, Langa, Cape

More information

ACADRI 2015 TRAINING PROGRAMMES

ACADRI 2015 TRAINING PROGRAMMES No. COURSE TITLE DATES VENUES SECRETARIAL AND GENERAL ADMINISTRATION 1. SKILLS ENHANCEMENT PROGRAMME FOR EXECUTIVE SECRETARIES AND ADMINISTRATIVE/ PERSONAL ASSISTANTS Jan 12 30, 2015 (3 wks) May 11 29,

More information

Integrated Logistics System (ILS) Procedures Manual

Integrated Logistics System (ILS) Procedures Manual THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE (ILS) Procedures Manual Roll-Out Version September 2008 ACRONYMS Term English Swahili ARV Anti-Retroviral (drug) Dawa ya kupunguza

More information

The Nguzo Saba of the seven days of Kwanzaa:

The Nguzo Saba of the seven days of Kwanzaa: The 7 principles of Kwanzaa Theme 1 Umoja (oo-mo-jah) Unity stresses the importance of togetherness for the family and the community, which is reflected in the African saying, "I am We," or "I am because

More information

The Story of Swahili

The Story of Swahili The Story of Swahili John M. Mugane OHIO UNIVERSITY PRESS ATHENS, OHIO in association with the OHIO UNIVERSITY CENTER FOR INTERNATIONAL STUDIES Athens CONTENTS List of Illustrations Acknowledgments ONE

More information

Your Rights and Responsibilities

Your Rights and Responsibilities Your Rights and Responsibilities A Charter for Consumers of the South Australian Public Health System National Library of Australia Cataloguing-in-Publication entry Title: Your rights and responsibilities

More information

23 280 ก ก 2558. ก ก Hydrologic Cycle

23 280 ก ก 2558. ก ก Hydrologic Cycle ก 23 28 ก ก 2558 ก ก Hydrologic Cycle ก. ก ก ก ก. ก... ก 65-5533-46-5533-47 ก - ก - 8 ก ก ก ก ก 12-46 ก 17 1 ก ก ก ก ก ก ก 1. ก ก 25 2. ก ก ก ก ก 3. ก ก ก ก ก ก 4. ก ก ก ก 5. 1 31 - 1. ก. ก 2 2. P.7A..

More information

LIN892: Distributed Morphology

LIN892: Distributed Morphology Simba & Rafiki, Hakuna Matata: Nominal Coordination and Noun Class Agreement in Swahili Ai Taniguchi (taniguc7@msuedu) April 30, 2013 :* *: :* *: :* *: :* *: :* 1 Overview What happens when you conjoin

More information

CURRICULUM VITAE. 1. SUMMARY OF EXPERIENCE Special Needs Education Lecturer Psycho-educational Assessment Professional

CURRICULUM VITAE. 1. SUMMARY OF EXPERIENCE Special Needs Education Lecturer Psycho-educational Assessment Professional CURRICULUM VITAE NAME CURRENT POSITION UNIVERSITY ACADEMIC POSITION INSTITUTION PHYSICAL ADDRESS WANYERA SAMUEL Coordinator Special Needs Education Research Laboratory Project Lecturer Special Needs Education

More information

Lesson 9: Swahili Noun Classes

Lesson 9: Swahili Noun Classes Lesson 9: Swahili Noun Classes Noun Classes [ngeli za Kiswahili] Nouns in Kiswahili are grouped into various noun classes because of two main reasons: 1. their characteristics as a noun 2. Kiswahili s

More information

Primary Care Plus Enrollment Booklet

Primary Care Plus Enrollment Booklet Primary Care Plus Enrollment Booklet 1 Table of Contents Welcome to Primary Care Plus (PC Plus)!... 3 What is PC Plus?... 3 Medicaid or Dr. Dynasaur Managed Care... 3 Important:... 3 How to join PC Plus...

More information

V-TO-I MOVEMENT IN KISWAHILI

V-TO-I MOVEMENT IN KISWAHILI AAP 55 {1998).. 129-144 V-TO-I MOVEMENT IN KISWAHILI DEO NGONY ANI Introduction In recent years, the Bantu oject affix that is commonly known as the oject marker (OM) 1 has attracted considerale deate

More information

MOSHI UNIVERSITY COLLEGE OF CO-OPERATIVE AND BUSINESS STUDIES (MUCCoBS) A Constituent College of Sokoine University of Agriculture

MOSHI UNIVERSITY COLLEGE OF CO-OPERATIVE AND BUSINESS STUDIES (MUCCoBS) A Constituent College of Sokoine University of Agriculture MOSHI UNIVERSITY COLLEGE OF CO-OPERATIVE AND BUSINESS STUDIES (MUCCoBS) A Constituent College of Sokoine University of Agriculture PROSPECTUS 0 ABBREVIATIONS AND ACRONYMS ACC ADB ADCA ADCM AMU BA-AF BA-BEC

More information

Tense and aspect in Swahili

Tense and aspect in Swahili UPPSALA UNIVERSITET D-uppsats Institutionen för lingvistik HT 2003 Tense and aspect in Swahili Anna-Lena Lindfors Handledare: Anju Saxena 2 Contents Abbreviations 1. Introduction 2. Background 2.1 The

More information

Vidunda (G38) as an Endangered Language?

Vidunda (G38) as an Endangered Language? Vidunda (G38) as an Endangered Language? Karsten Legère University of Gothenburg 1. The position of Swahili and other Tanzanian languages Tanzania is a multi-ethnic and, as a consequence, multi-lingual

More information

Lourenco Noronha. Lektor (1974-2009 für Swahili Literatur am Institut für Afrikawissenschaften der Universität Wien

Lourenco Noronha. Lektor (1974-2009 für Swahili Literatur am Institut für Afrikawissenschaften der Universität Wien Lourenco Noronha Lektor (1974-2009 für Swahili Literatur am Institut für Afrikawissenschaften der Universität Wien SWAHILI-LITERATURLISTE: SEKUNDÄRLITERATUR Stand: November 2007 1 Vorwort Dibaji Ich hatte

More information

ORODHA YA TAASISI/MAKAMPUNI

ORODHA YA TAASISI/MAKAMPUNI ORODHA YA TAASISI/MAKAMPUNI S/N0. JINA /TAASISI/KAMPUNI SIMU 1. Director General +255 22 2123583-4 TASAF 2. Director General, +255 22 2126516 WAMA 3. The Chairman, +255 22 2122651 TACAIDS 4. Executive

More information